Zikiwa zimesalia siku 7 tu, dirisha dogo la usajili barani ulaya kufungwa. Baadhi ya timu (na wachezaji) bado zinajitafakari kabla ya kufanya maamuzi.
Kule Old Trafford, Jesse Lingard anasubiri uamuzi wa bodi ya wakurugenzi wa Manchester United. Hii ni baada ya kocha Ole Gunnar Solskjaer kumkubalia ombi lake la kutaka kusajiliwa mwezi huu lakini bado bodi haijapitisha ombi hilo.
West Ham United ndio timu inayotajwa kutaka kumsajili Jesse Lingard, atafanikiwa?
Pale darajani, Billy Gilmour naye anasubiri hatma yake kwenye dirisha hili la usajili. Kocha Frank Lampard haoni kinda huyu akitolewa kwa mkopo mwezi huu lakini mchezaji huyu anahitaji kupata muda wa kucheza zaidi na hivyo kuondoka Chelsea ndani ya siku 7 zilizobaki ni suluhisho sahihi kwake.
Mikel Arteta amepunguza mzigo kwenye kikosi chake baada ya kuwaondoa Mesut Ozil na Sokratis kwenye dirisha hili la usajili. Kuondoka kwa wawili kunatajwa kuwa njia ya mmoja kuingia. Arsenal wanatajwa kuwa mbioni kumshuka Martin Odergaad kutoka Real Madrid.
Licha ya kutua Spurs kwa mkataba wa miezi 18, Gerdson Fernandes hana namba kwenye kikosi cha Mourinho na sasa anahusishwa na klabu ya Torino kule Serie A. Hapa ndio kunautata kidogo, kimsingi inabidi Benfica wakatishe mkataba na Tottenham ili Fernandes arudi Ureno na kisha Torino watamchukua kutoka huko na sio Spurs.
Anayejaribu hawezi kutoka kapa Meridianbet! Kasino ya mtandaoni ya Meridianbet inakuhakikishia ushindi mkubwa kila unapojaribu kuingia mchezoni. Washindi hushindana, ingia mchezoni!
Ernest Kimeru
Jesse Lingard bora asepe tuu Man U hana chake
Magdalena
Tena wafanye maamuzi ya haraka
Dorophina
Siku zimeisha klabu nyingi hazijafanya usajili wa maana
Adelta
Wafanye maamuzi yaliyo sahii
Sadick
Jesse Lingard hana ubora wa kucheza Man U na Billy Gilmour anatakiwa kupewa muda zaidi Chelsea
Venerose
Wanatakiwa umakini wa hali ya juu
Mwanahamisi
Wajitahidi wafanye maamuzi yaliyo sahihi
Sarah
Wafanye maamuzi kwausahihi
Sania
Usajili unapasua vichwa
Hopemwaikuka
Mmh
Shakila mrope
Duh wanatakiwa wawe makini
Rahmal
Sa itakuwaje
Latifa juma mohamed
Umakini wa Hali ya juu watakiwa.
Angelina
Nice update
Lydia Emmanuel Magoti
Wafanye mamuzi haraka
Issa
Ngoja tuone