Timu zitaruhusiwa kufanya mabadiliko matano ya wachezaji kwa mechi baada ya International Football Association Board (IFAB) kufanya mabadiliko ya muda kwenye sheria za mpira ili kuendana hali ya kurejea kwa Ligi baada ya Corona kulazimisha Ligi nyingi kusimama.

FIFA ilishauri sheria hiyo kufanyiwa mabadiliko na IFAB, ambao ndio wenye jukumu la sheria za mchezo, wakati wachezaji watakapocheza mechi kwa muda maalum kipindi cha miezi ya kiangazi.
Timu zitakuwa na nafasi tatu wakati wa mechi kufanya mabadiliko na pia wakati wa mapumziko, ili kuzuia mpira kusimama bila kila mara. Katika mashindano yenye muda wa ziada pia itakuwa hivyo, mchezaji ambae hajaingia ataruhusiwa kuingia.
Mabdiliko haya ya sheria yameanza mara moja, lakini kwenye mashindano binafsi wataamua kama wataiga mfumo huu. Itatumika Bundesliga, ambayo imepangwa kuanza May 16 japo bila mashabiki.

Kwasasa, La Liga na Shirikisho la Hispania wamekubaliana kutumia sub tano kwenye mechi zote zilizosalia, ambayo inatarajia kuanza Juni.
IFAB imesema mabadiliko haya yatatumika kwenye mashindano ambayo yamepangwa kumalizika kabla mwaka huu haujaisha, na mapitia yatafanyika hapo baadae kuona kama tunaweza kuendelea na mabadiliko hayo msimu ujao.
IFAB wamebadili sheria zake kuhusu VAR kuruhusu mashindano yote ambayo yanatumia teckonolojia hiyo kuacha kutumia, watakapoendelea na msimu.
Premier League itajadili kuhusu mabadiliko hayo na vilabu, japo kuna lengo la kuachana na VAR.



Gabriel
IFAB Sheri’s zao zko vzur kulingana kipindi hiki
Shafii
Ifab Sheria zao zinaua ladha ya mpira
Frank Patrick
Aisee bora VAR ifutwe tu inaharibu sana radha ya mpira
Asia Abdy
Itabid tu kufanya mabadiliko kutokana na kipind hk kigum no way
Rehema Dickson
AVR imekuja me kumaliza Radha yote ya mpira sheria mpya kila kukicha
Furahav
Itakuwa safi sana.
Zainabu
Iwe ivyo tu ilaumiwe corona
mwakalosi
itatoa nafasi ya wachezaji wengi
tahiya
itakuwa poaw
Mwajuma
Bora VR zinazingua sana
Hamidu
Kwangu me VAR ufutwe kabisa ..kwasababu ikiwepo inanyima radha ya mchezo .
Nasra
VAR isifutwe inasaidia Sana
Neema juma
Bora VAR ifutwe tu
Khadija
VAR isifutwe inasaidia sana
SADICK
VAR ililetwa kumusaidia refa lakini wakati fulani maamuzi yanakuwa na utata mkubwa mno. Hakuna sababu ya kuendelea nayo. Asante IFAB
Elika
Sasa si waifute tu jamani
Neema hassan
Itakuwa vizuri saana
Adelta
Bora var ifutwe
mathayo sonje
sab tano? aisee itakaa poa sana alafu na hiyo VAR itolewe tuu inazingua japo wakati mwingine inasaidia
Jenifer
Bora tu mabadiriko yafanyike hakuna namna
Lydia Emmanuel Magoti
Itakuwa poa sana
Emmy cleopa
Itakuwa vizur sana
Rehema
Safi sn
Pove
IFAB wamefany jamb la maana sana kwa kpnd hch dunia inabambana na janga la korona
Swai
IFAB wamefanya Jambo la busara kubadili Sheria kwa kipindi hiki Cha janga hili la COVID-19
felister
wapunguze sub bana
Ester mmakasa
Wamefanya maamuzi mazuri ili viwango vya wachezaji wetu visishuke.
Kenani
Mi kote kote naona sawa muda mwingine nzur muda mwingine inazngua
Lombo
sheria znaua soka bhn
Ernest Kimeru
Kisimamishwa kwa VAR sio jambo zuri sana japo kunawakati inaleta kizungumkuti katika maamuzi lakini ni tekinolojia bora sana kwa upande wa kuwasaidia marefa katika kufanya maamuzi.
Njiku
VAR ipo poa sanaa
Adelta
Bora var ifutwe
Asha
Itakuwa vzr sana
Asha
Itakuwa vzr sana
aisha
VAR .isifutwe
Fatina
Waache 2
Theckla
Kila kitu kina uzuri wake na kasoro zake, km kuna muda tunaona VAR inafanya sahihi na tunafurahia iwenye tushindwe kukubali mapungufu yake?
David pere
Var ilikuwa inapunguza burudani sana
farida ahmadi
Itakuwa vzr Sana