Varane: Najua ni kwanini Casemiro kachagua Man Utd.

Casemiro alitambulishwa kwenye Uwanja wa Old Trafford kabla ya Manchester United kushinda 2-1 dhidi ya Liverpool Jumatatu usiku. Mbrazil huyo amesaini mkataba wa miaka minne katika klabu hiyo, kufuatia mwenzake wa zamani wa Real Madrid Raphael Varane kuhama kutoka mji mkuu wa Hispania kwenda Manchester. Varane anaamini kwamba sifa za kiungo huyo wa kati mwenye umri wa miaka 30 “shujaa” zitafaa kuisaidia timu hiyo.

Raphael Varane alisema “anajua hasa kwanini” kiungo wa kati wa Brazil Casemiro aliamua kujiunga na Manchester United kutoka Real Madrid.

Wawili hao walitumia misimu saba pamoja katika klabu ya Real Madrid, na kuisaidia klabu hiyo kutwaa mataji manne ya Ligi ya Mabingwa.

Na Varane alifichua kwamba anaelewa kabisa kwanini Casemiro alitafuta changamoto mpya.
“Nadhani hahitaji usaidizi wangu kufanya chaguo lake,” Varane alisema kuhusu uamuzi wa mchezaji huyo wa miaka 30 kuhamia Man Utd. “Ninajua haswa anachohisi na kwanini anakuja hapa baada ya kile alichoishi Madrid.

Makala iliyopita

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.