Ligi Kuu Uingereza – EPL yazidi kupamba moto kwa vilabu vinavyopambana kuendelea kubaki kwenye ligi hiyo msimu ujao.
Baada ya kipigo cha Watford kutoka kwa Manchester City na Aston Villa kumchakaza Arsenal, timu hizi zinakuwa sawa kwa pointi wakiwa na tofauti ndogo ya magoli ya kufungwa na kufunga. Aston Villa wamepanda kwa nafasi moja wakiwa nafasi ya 17 wakati Watford wanashika nafasi ya 18.
Goli la Trezeguet katika kipindi cha kwanza lilitosha kupeleka matumaini ya kusalia kwenye EPL kwa mashabiki wa timu ya Aston Villa na kuwatoa katika nafasi ya kushuka daraja ambayo waliishikilia tangu tarehe 28 mwezi Februari, 2020.
Upande wa pili, Westham United wakiwa katika nafasi ya 16 kwenye msimamo wa EPL watakutana na Manchester United leo ale Old Trafford. Woganga nyundo hawa wa London wanahitaji pointi 1 tu kujiweka katika nafasi nzuri ya kusalia kwenye ligi kuu msimu ujao wakiwa na tofauti kubwa ya magoli kati yao na Aston Villa, Watford na Bournemouth.
Kocha wa Aston Villa alisema ” Tuliwaona Watford wakicheza mapema na kufungwa. Tulijua tunahitaji ushindi ili angalau tuwafikie. Kwa ushindi huu, hatima ya kusalia ligi kuu ipo mikononi kwetu”
Kwa kipigo hiki kwa Arsenal, ni dhahiri kwamba kikosi cha Mikel Arteta hakiwezi kumaliza katika nafasi 6 za juu kwenye msimamo wa ligi kuu msimu huu. Hii ni mara ya kwanza kwa miaka 25.
Siku ya jumapili itakuwa ndio siku ya kujua mbivu na mbichi katika kumaliza msimu huu wa Ligi Kuu Uingereza. Aston Villa atakutana na Westham United, Arsenal uso kwa uso na Watford wakati Everton atamenyana na Bournemouth. Nani anashuka na nani anasalia Ligi Kuu?
Kwa sababu ya thamani ya pesa yako, kwa kila muamala unaofanya wa kuweka pesa kwenye akaunti yako ya Meridianbet unapata 5% bonasi.
Rehema
Bonge la makala
Mwanahamisi
Asante kwa taarifa
Ester jackson
Kwel ni vita ambayo havijulikani nani atashinda
Khadija
Hebu tuone nani mshind maana ss mashabiki yetu macho#meridianbettz
Angelina
Goodupdate
Magdalena
United Nina Imani anaweza kushindwa mechi ya Leo maana sizani kama atakuwa tayari kupoteza nafasi
Zeiyana
Itakua mtanange wa kukata na shoka
Samiah
Gud news
Johnmary joel
Hii ni nivutanikuvute#meridianbett
caroline
kwa kweli ngoma ngumu
Fatina mfingi
Makala nzur
Sylvester
Klabu nne za chini zitapambana ipasavyo ili visiweze kushuka daraja isipokua Norwich ambao wameshahakikiwa kushuka daraja,Aston Villa,Watford,Bournemouth mmojawapo ananafasi ya kusalia ligi kuu ingawa nafasi kubwa ipo kwa Aston Villa na Watford hivyo basi mechi za jumapili zitakua za kukata na shoka.
Dorophina
Man u hawawezi kukubali kupoteza mechi ya leo maana kumekuwa na mvutano wa kupanda daraja
Mariam mtandama
Makala mazur
felister
hiyo kweli ni vita ambapo majibu yake ni kitendawili
Njiku
Hii kitu ndio tuliokuwa tunapenda kuiona kuwa aston villa apambane na kubaki EPL ila anatakiwa kukazaa butii ili kufanya vizuri ili kuendelea kusalia EPL
Adelta
Mechi hii
Tusubiri matokeo
aisha
Ama kweli.ni vita ya sintofaham kuwa nani atashinda
Neema juma
Nasubiriaa kushuhudia kwa hamu
Samira
Makala safi sana hii
Rose kapinga
Mwisho was mechi kitaeleweka tuu
Sadick
Wiki ya kuona matokeo ya kushangaza katika mechi za Aston Villa, Westham and Watford. Kila inayokutana na timu hizi itarajie mchezo mgumu#meridianbettz
Zuhura omary kindamba
Nasubili kuona nn kitatokea ndani ya dk 90
David Pere
Kwa mtazamo wangu Mimi naona Aston villa watabaki EPL bila Shaka kabisa
Janeflora malisa
Nice
devotha
asante kwa makala
Shafii
Ni wakati wa makocha kuumiza vichwa kwani kila mmoja wao anataka kusalia kwenye ligi kuu hapo msimu kesho.
Issa
Villa bado wana nafasi ya kubaki epl washinde mech zilizobaki
Saupha mohamed
Good news
Amani
katika mechi za Aston Villa, Westham and Watford. Kila inayokutana na timu hizi itarajie mchezo mgumu#meridianbettz
Gabriel
Habar njema
farida ahmadi
Habari njema Sana
Asia Abdy
Tunasubir tuone
Theonestina
Itakuwa bonge la mechi maana wote wakali
Amiri Kayera
Mechi za mwish zitaamua
Hope mwaikuka
Hili balaa
Genia Sikaluzwe
Ahsant kwa taarifa
Revina
Hii ndo hiyo ilikuwa inahitajika kufahamika,na ni habari njema
mwakalosi
Aston villa anabaki aisee
mwajumah
Nice#Meridianbettz
Ernest
Napata mashaka kwa Aston Villa kubaki ligi kuu
Lydia Emmanuel Magoti
Mtanange watari ulikuwa
Furahav
Tusubili tuone nani atashuka.