VITA YA YANGA NA FOUNTAIN GATE NI KESHO ARUSHA

Siku moja pekee imesalia kabla ya Fountain Gate FC kuwa wenyeji wa mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga SC, kwenye vita ya kuwania alama tatu kwenye mchezo utakaochezwa kesho Juni 18 kwenye Uwanja wa Shekh Amri Abeid Kaluta.

VITA YA YANGA NA FOUNTAIN GATE NI KESHO ARUSHA

 

Yanga walipaa kwa ndege jana asubuhi kwenda Arusha na jana hiyo hiyo wakapata nafasi ya kufanya mazoezi ya kwanza wakiwa jijini humo.

Na ripoto ya Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe alisema: “Tunamshukuru Mungu kuwa kila kitu kipo sawa hapa Arusha, siyo mchezo mwingine rahisi, lakini tumekuja na dhamira ya kushindana na kushinda mchezo huu.”

Kikosi hicho kiliondoka kikiwa katika hali nzuri ya kujiamini baada ya kuendelea kufanya vizuri kwenye mbio za ubingwa, huku benchi la ufundi likisisitiza umuhimu wa kushinda mechi zote zilizosalia ili kutimiza malengo ya msimu huu.

Wachezaji wa Yanga walionekana wenye furaha na morali ya juu walipokuwa wakijiandaa na safari hiyo, ishara ya utayari wao wa kukabiliana na changamoto ya mchezo huo ambao unasubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa soka nchini.

Wananchi wanaingia katika pambano hilo wakilenga kuendeleza matokeo yao mazuri ya msimu huu pamoja na kuimarisha nafasi yao kileleni mwa msimamo wa ligi, wakati mbio za ubingwa zikizidi kupamba moto kuelekea tamati ya msimu.

VITA YA YANGA NA FOUNTAIN GATE NI KESHO ARUSHA

Kwa upande wa Fountain Gate FC, mchezo huo unaonekana kuwa fursa adhimu ya kupima uwezo wao dhidi ya moja ya timu zenye mafanikio makubwa nchini, jambo linalotarajiwa kuongeza ushindani mkubwa ndani ya dakika 90 za mchezo.

Kocha Mkuu wa Yanga, Abdihamid Moalin, ameendelea kuwakumbusha wachezaji wake umuhimu wa kubaki makini na kutoridhika na mafanikio ya hivi karibuni, akisisitiza kuwa kila mechi iliyobaki ni sawa na fainali katika harakati za kutetea taji la ligi.

Mashabiki wa Yanga kutoka Arusha na mikoa ya jirani wanatarajiwa kujitokeza kwa wingi katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid kuipa sapoti timu yao, huku Wananchi wakisaka ushindi mwingine muhimu utakaowasogeza hatua zaidi kuelekea kutetea ubingwa wao.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.