Wachezaji 3 Scotland Wapata Covid-19.


Wachezaji Stuart Armstrong, Kieran Tierney na Ryan Christie wa timu ya taifa ya Scotland watakosa nusu-fainali ya mchujo wa kufuzu kwa fainali za Euro 2021 dhidi ya Israel kwa sababu ya Covid-19.

Japo Armstrong ndiye wa pekee aliyepatikana na virusi vya corona, Tierney ambaye ni beki wa Arsenal na Christie wa Celtic watalazimika kujitenga kwa siku 14 zijazo kwa kuwa walikuwa na Armstrong pamoja mazoezini.

 

Wachezaji 3 Scotland Wapata Covid-19.

Wachezaji hao hawatakuwa pia sehemu ya kikosi cha Scotland kitakachoshiriki mechi za Nations League dhidi ya Slovakia na Jamhuri ya Czech.

Christie atakosa pia mechi itakayowakutanisha Celtic na Rangers mnamo Oktoba 17, 2020 huku Tierney akitarajiwa kukosa mchezo wa Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) litakalowakutanisha na Manchester City siku hiyo hiyo.

Armstrong ambaye ni kiungo wa Southampton, hakupatikana na virusi vya corona alipowasili katika kambi ya Scotland mnamo Oktoba 5, 2020.

 

Wachezaji 3 Scotland Wapata Covid-19.

Hata hivyo, vipimo vya afya vilivyofanywa na Shirikisho la Soka la bara Ulaya (Uefa) vilibainisha kwamba mchezaji huyo alikuwa anaugua Covid-19 na hivyo atajitenga kwa siku 10 kuanzia Oktoba 6, 2020.

“Ingawa hizi ni taarifa za kuvunja moyo, muhimu zaidi ni kuzingatia kanuni zilizopo za afya na kuhakikisha kwamba wachezaji wengine wanasalia katika hali nzuri,” akasema kocha wa Scotland, Steve Clarke.


Weka Pesa kwa Airtel Money!

Sasa unaweza kuweka pesa moja kwa moja kwenye akunti yako ya Meridianbet kwa kutumia mtandao wa Airtel. Usipate wasi wasi, tunaifanya kazi kuwa rahisi zaidi!

Soma Zaidi

35 Komentara

    Duuuh hii ni hatari

    Jibu

    Corona noma

    Jibu

    Covid19 bado ni tishio kwa wenzetu wazid kuchukua tahadhari

    Jibu

    Wanatakiwa wawe makini na hili janga

    Jibu

    Pole yao

    Jibu

    Hili gojwa Ni hatari sana wanatakiwa waendelee kujikinga pole yao

    Jibu

    huu ugonjwa unazidi kuleta gumzo kali sana jamani

    Jibu

    Umakin unaitajika san dhid ya ili janga

    Jibu

    Huu ugonjwa unaendelea kuwa tishio kubwa nchi za wenzetu

    Jibu

    Duu pole yao

    Jibu

    Sad newz

    Jibu

    Poleni sana duuh covid 19 ni hatari sana

    Jibu

    Duuh pole yao

    Jibu

    Pole yao

    Jibu

    Pole sana kwao..huu ugonjwa sio poa

    Jibu

    Pole yao

    Jibu

    Pole yao

    Jibu

    Huu ugonjwa bado no janga la dunia

    Jibu

    Corona inakatsh San shughur za michez

    Jibu

    Pole yao

    Jibu

    Corona sio poa

    Jibu

    Pole yao

    Jibu

    Duuh waugue pole

    Jibu

    Pole yao

    Jibu

    Habar ya kusikitisha sana

    Jibu

    duh wajifushe nyungu kama vipi

    Jibu

    Pengo kubwa

    Jibu

    Duuuh

    Jibu

    Pole maan hapo ni mtian mkbwa

    Jibu

    Corona sio pouwa

    Jibu

    Duuh atarii sana

    Jibu

    Covid 19 ni balaa lingine

    Jibu

    Dah! So sad

    Jibu

    Duh majanga kwl

    Jibu

    Wachezaji hao hawatakuwa pia sehemu ya kikosi cha Scotland kitakachoshiriki mechi za Nations League dhidi ya Slovakia na Jamhuri ya Czech.

    Jibu

Acha ujumbe