Waliotoka Ujerumani Wakawika Premier League

Kura yako kwa nani hasa? Je, ni Ozil? Klinsmann? Au Sane? Hebu jichagulie mchezaji wako aliyetisha zaidi akiwa mwanasoka wa Ligi Kuu ya Uingereza akitokea taifa kubwa la Ujerumani.

Lakini, hebu kwanza, kabla hatujafika huko tuangalie takwimu za wachezaji wa taifa hilo tukihusisha na ushiriki wao kwenye Premier League.

Kwa sasa tunasherehekea mafanikio yao waliyoyapata wakiwa na klabu za Uingereza katika nyakati mbalimbali. Wamekuwa na vipaji vya hali ya juu sana. Na tungependa mno kujua mtazamo wako wa nani ni mkali kati yao.

Kumekuwa na jumla ya wanasoka 69 waliocheza ndani ya Premier League tangu pale Matthias Breitkreutz alipotokea benchi akiichezea klabu ya soka ya Aston Villa waliokuwa wakicheza dhidi ya Manchester City mnamo mwezi Desemba mwaka 1992.

Uwe Rosler alikuwa ni Mjerumani wa kwanza kufunga bao katika michuano hiyo wakati alipoifungia timu ya soka ya Man City mwezi Machi mwaka 1994.

Miezi michache tu baadaye naye Jurgen Klinsmann akajiunga na klabu ya Tottenham Hotspur na kufanikiwa kufanya makubwa sana wakiwa pamoja pale alipofunga bao katika gemu yake ya kwanza na kusaidia sana katika ushindi mnono wa magoli 4-3 wakiwa pale kwa Sheffield Wednesday.

Ukitazama takwimu za assists, anayekamatia kilele cha wote miongoni mwao, kwa hakika ni Mesut Ozil akiwa ametoa jumla ya pasi 54 za magoli.

Kumi na tisa kati yake alizifikia katika msimu mmoja wa ligi, mwaka 2015/16, na hapo anakuwa amezidiwa na mwanakabumbu Thierry Henry, ambaye alifikisha jumla ya magoli 20 katika msimu wa mwaka 2002/03.

Pia, Ozil anashikilia rekodi ya kuwa na magoli mengi zaidi yaliyofungwa na mchezaji kutokea taifa la Ujerumani katika michuano hiyo, anawazidi magoli manne akina Klinsmann pamoja na mwenzake Rosler.

Wachezaji wawili ambao walicheza nafasi ya mido wakafanya poa sana kwenye Premier League kabla ya ujio wa Ozil mwezi Septemba mwaka 2013 walikuwa ni Dietmar Hamann pamoja na Michael Ballack.

Hamann anakaa kwenye nafasi ya pili nyuma ya mwenzake Robert Huth katika orodha ya wachezaji walioingia uwanjani kwa muda wote kutokea Ujerumani, amecheza jumla ya mechi 268 akiwa na klabu za soka za Newcastle United, Liverpool pamoja na ile ya Man City.

Ballack alidumu katika klabu moja pekee katika mashindano hayo na kusaidia klabu ya soka ya Chelsea kushinda taji msimu wa mwaka 2009/10 akiwa na uzoefu na umaridadi mkubwa sana kwenye taaluma yake hiyo.

Takwimu zinazoongoza kutoka kwa wachezaji wa Ujerumani waliohudumu PL

MechiMagoliAssists
Robert Huth322Mesut Ozil33Mesut Ozil54
Dietmar Hamann268Jurgen Klinsmann29Leroy Sane28
Mesut Ozil184Uwe Rosler29Dietmar Hamann22
Per Mertesacker156Leroy Sane25Christian Ziege18
Jens Lehmann148Robert Huth21Thomas Hitzlsperger17

 

Kwa miaka ya hivi karibuni, Wajerumani wawili wamefanya makubwa sana kwa kikosi cha meneja mkali Pep Guardiola pale Man City.

Ubora na umachachari wa mchezaji Leroy Sane uliifanikisha sana klabu ya City kutwaa taji katika kampeni zao za msimu wa mwaka 2017/18 na ule wa mwaka 2018/19, wakati ambapo mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 alichangia upatikanaji wa mabao 25 na kutoa pasi 28 za magoli katika mechi 89 mpaka sasa.

Mchezaji mwingine, Ilkay Gundogan naye pia amekuwa mtu wa muhimu sana kwa kikosi hicho tangu awasili klabuni pale mnamo mwezi Juni mwaka 2016.

Kwenye takwimu za magoli, Jens Lehmann alitisha sana akiwa na Arsenal katika msimu wao wa “Invincible” mwaka 2003/04, pale alipoweka clean sheets 15 kwa ujumla wake.

Nafasi ni yako sasa kutazama takwimu hizo hapo juu na kuangalia mabao maridadi kabisa kutoka kwa Wajerumani waliohudumu ndani ya EPL kabla hujatuambia ni nani kati yao anastahili kuwa mfalme wao:

  • Michael Ballack
  • Ilkay Gundogan
  • Dietmar Hamann
  • Jurgen Klinsmann
  • Jens Lehmann
  • Mesut Ozil
  • Leroy Sane

32 Komentara

    Sane talent player.# meridianbettz

    Jibu

    Asanteni meridianbet kwa taarifa

    Jibu

    Michael Ballack bonge la player alikiwasha sana Chelsea pale

    Jibu

    Ozil hanajua mpira ila hajawai kuchukua taji

    Jibu

    Asante meridianbet kwa kutujuza

    Jibu

    Per mertesacker moja ya mlinzi Bora epl na ujerumani moja ya vitasa wangu na wakubal ni mtu wakaz sana mjerumani mashine thanks meridian kwa update

    Jibu

    Ozil mtu mbaya

    Jibu

    Ozili Yuko juu bwana

    Jibu

    German players uwa wapo vizuri sana popote watakapoenda wanakiwasha

    Jibu

    Habari njema

    Jibu

    Asante meridianbet kwa taharifa

    Jibu

    Wamefanya makubwa sana hao watu EPL sio ligi ya kitoto hongera zao

    Jibu

    Namkubali sana ozil

    Jibu

    Hatari sana

    Jibu

    Gundogan moto wa kuotea mbali

    Jibu

    Jurgen Klinsmann ndio kwangu bora anaieshi #meridianbettz

    Jibu

    Noma sana hyu mtu

    Jibu

    Habari za michezo napata meridian na pesa pia napata kwel mko vizuri

    Jibu

    Kwangu mimi Michael Ballack alikuwa bora. Asante meridianbet kwa makala nzuri.

    Jibu

    Ballack alikuwa mtu hatari kipindi chake pale Stamford Bridge

    Jibu

    Ozil yuko vizuri#asante meridianbet kwa makala

    Jibu

    Meridian mpo vizuri

    Jibu

    Ozil anaweza

    Jibu

    Mafundii

    Jibu

    Mie namkubali ozil jamani

    Jibu

    Ozil namkubali sana

    Jibu

    gud newz asante

    Jibu

    Kwa upande wangu ozil ni bora zaidi

    Jibu

    asanteni meridian kwa makala nzuri

    Jibu

    Ozil anatisha.

    Jibu

    Ozil alitisha

    Jibu

    Ozil mtu mbaya Yuko vzr hanajua Sana mpira

    Jibu

Acha ujumbe