Shabiki wa utotoni wa Chelsea, Nick Candy amejadiliana kuhusu kuunganisha nguvu na muungano unaojumuisha Todd Boehly, Jonathan Goldstein na Hansjorg Wyss; huku wamiliki wa Chicago Cubs, familia ya Ricketts na mfanyabiashara bilionea Ken Griffin watawasilisha zabuni.
Taarifa zinasema matajiri wanaoshindana kuinunua klabu ya Chelsea wanataka kuungana na kuongeza nguvu na uwezo wao wa ushawishi kifedha kuinunua klabu hiyo kuelekea tarehe ya mwisho, Ijumaa.
Kwa mujibu wa Sky Sports, mazungumzo ambayo yameanzishwa na kati ya Nick Candy pamoja na Todd Boehly, Jonathan Goldstein naHansjorg Wyss yanaendelea.
Familia ya Ricketts, ambayo inamiliki Chicago Cub tayari walifanya muungano wa kushirikiana katika ununuzi wa klabu hiyo.
Candy ambaye anatajwa kuwa na na pesa ya kutosha kuinunua klabu tayari alishawaahidi mashabiki kiti chao kwenye bodi ikiwa zabuni yake itakubaliwa.
Washindani wake wa karibu sasa wameamua kuungana naye kwa kuwa anafahamika kama shabioki wa muda mrefu wa Chelsea na uwezo wake wa kuendeleza biashara huko London.
SHAOLIN FORTUNES 100 ONJA LADHA YA USHINDI
Maana ya ushindi mkubwa ipo hapa katika mchezo wa SHAOLIN FORTUNES 100 ndani ya kasino maridhawa za meridianbettz. Kwa dau dogo unashinda zaidi, unaweza kucheza mara nyingi uwezavyo huku ukifurahia ladha ya ushindi.