Baada ya usafi kufanyika kwenye ngazi ya idara za uongozi ndani ya Manchester United, sasa kazi imehamia kwa wachezaji, wawili kuwekwa sokoni.
Manchester United ni miongoni mwa vilabu vyenye idadi kubwa ya wachezaji kwenye kikosi chao. Licha ya wingi wao, ni wachezaji wachache wanaopata namba kikosini hapo huku wengi wao wakiwa wanasugua benchi.
Idara ya ulinzi kushuhudia wachezaji wawili wakiwekwa sokoni kuelekea dirisha kubwa la usajili. Aaron Wan-Bissaka na Erick Bailly wanaripotiwa kuwa sokoni. Hii ni baada ya wachezaji hawa kutokuwepo kwenye mipango ya kocha Erik Ten Hag ambaye anatarajia kuchukua timu mwishoni mwa msimu huu.
Licha ya Bailly kuwa amesaini mkataba mpya miezi kadhaa iliyopita, sasa anaunganishwa na Bissaka kwenye orodha ya wachezaji ambao, M16 ipo tayari kupokea ofa za usajili wa moja kwa moja au, mkopo wenye kipengele cha kuwanunua moja kwa moja.
Kazi imeanza!
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.