Arsene Wenger anaunganishwa na Phil Neville kuwania kibarua Inter Miami.
Safari ya Inter Miami kumsaka meneja mpya baada ya kumalizana na Diego Alonso inaendelea kunoga, orodha ikiendelea kupamba mameneja wazoefu na walippata mafanikio makubwa katika soka.
Kwa mujibu wa ripoti za soka, meneja anayeachana na timu ya wanawake ya Uingereza Phil Neville ndiye anayepigiwa upatu zaidi kuwa kwenye mazingira mazuri na kibarua hicho.
Hata hivyo, Inter Miami ambao wanashiriki ligi ya MLS wanaendelea kutazama meneja bora atakayewafaa na wana machaguo kadhaa mezani, Arsene Wenger, Robbie Keane na Bob Bradley wakiwa kwenye orodha.
Neville ambaye anaonekana kuwa kwenye nafasi nzuri zaidi natajwa kuwa anatazamia kumalizia jukumu lake kwenye timu ya taifa hado baada ya michuano ya Tokyo Olympics iliyoahirishwa.
Kuna taarifa kuwa licha ya kuwa Neville anataka kuondoka kwenye timu ya taifa ya wanawake ya Uingereza, huenda tofauti zake na Shirikisho la Soka zikamalizika na akasalia na kibarua chake, hii inamaana Arsene Wenger, Robbie Keane na Bob Bradley wanakuwa kwenye nafasi nzuri zaidi.
Ndio, kwetu Mteja ni mfalme. Jiunge sasa na familia ya Meridianbet bila malipo yeyote na sisi tutakuzawadia bonasi ya shilingi 3,500 kama sehemu ya kukukaribisha kwenye familia hii BURE!!!. Unasubiri nini??
Shakila mrope
Good New
Janeflora malisa
Safi
Adelta
Tusubiri tuone itakuwaje
Magdalena
Wenger anazingua
Ernest Kimeru
Watamuua Wenger kwa Pressure bure, Anatakiwa kurelax now ameshapata pressure kubwa sana wakati yupo Arsenal
Rahmal
Tunangojea tuone
lombo
vzr
Caroline
Arden Wenger yupo vizuri
Mwanahamisi
Safi
Hopemwaikuka
Wenger anafaa
aisha
Safi
Dorophina
Wenger yupo vizuri atawafaa
Lydia Emmanuel Magoti
Safiii
Issa
Wenger nenda inter
Saupha mohamed
Safi
warda
Wenger hakati tamaa