Inter Milan wanakumbana na wiki ngumu wakiwa wanajiandaa kuumana na AC Milan na huku wachezaji wake sita kwa sasa wakiwa na maambukizi ya Covid-19. Antonio Conte atakuwa na siku moja tu ya mazoezi ya kuandaa timu kwa pambano la Jumamosi.
Alessandro Bastoni, Milan Skriniar, Roberto Gagliardini, Radja Nainggolan, Ionut Radu na Ashley Young wamepatikana na Covid-19 na hawatastahili kucheza dhidi ya Milan Jumamosi wakati Stefano Sensi pia akiwa amesimamishwa.
Kwa mujibu wa La Gazzetta dello Sport, Bastoni anaweza kucheza ikiwa ikiwa akifanya tena vipimo siku ya Alhamisi na kupatikana bila maambukizi, zaidi ni afadhali ikiwa Serikali ya Italia inapunguza kipindi cha karantini hadi kuwa siku kumi.
Upana wa kikosi cha Inter Milan kitamruhusu Antonio Conte kupanga safu ya ushindani sana mnamo Jumamosi ikiwa hakutakuwa na taarifa nyingine mbaya katika siku zijazo.
Kulingana na Sky Sport, wachezaji wengi wa Inter ambao kwa sasa wako kwenye jukumu la Kimataifa watarudi kwenye kituo cha Suning siku ya Alhamisi wakati watakuwa na watafanyiwa vipimo.
Ikiwa wachezaji hawatapatikana na maambukizi zaidi, basi itakuwa ni afadhali kwa Conte katika kusuka kikosi kizito cha Inter Milan Jumamosi,
Naam, hapa ni mahali pako! Kuwa shujaa kwenye sloti hii ya Samurai Ken ujishindie mkwanja na kujipa burudani murua.



Elika
Kwakuwa Mungu yu pamoja nao watapona tu na watarejea vikosini
Zeiyana
Hii mechi kwa upande wa inter itakua ngumu sana
magdalena
huu ugonjwa Mungu tu atusaidie hakuna namna nyingine ya kuuzuia
Angelina
Wazid kuchukua tahadhari
Venerose
Inter wanatakiwa wawe na umoja
Neema
Wanatia huruma mno ila watakuwa sawa tu wasijali
Tatu
Watakaa sawa
Sauda
Habari mbaya kwa mashabiki wa Milan
aisha
Watakuwa sawa tuu kwa uwezo wa mungu
Dorophina
Inter wanakibarua kizito sana hiyo tarehe
Nasra
Inter kazi wanayo
Shani
Bonge la Derby ila inte wapo vizuri watapata matokeo
Genia Sikaluzwe
Habari mbaya kwa mashabiki wa Milan
Issa
Milan derby patachimbika
Mwanahamisi
Watakaa sawa
Ernest
Nadhani itakuwa vizuri kama mechi itahairishwa tuu
Amiri Kayera
Corona itafelisha Sana club nying
Caroline
Jmn corona mbona inasakama wachezaji
Mwajumah
Inter kazi wanayo
Janeflora malisa
Asnt kwa taarif
Saupha mohamed
Inter kazi wanayo
Gabriel
upande wa inter itakua ngumu sana
Sabrina
Duh hatarii hii
Povel
Mambo ni moto MILAN derby💪💪💪💪💪
Hopemwaikuka
Dah