Baada ya kushtushwa na uamuzi wa Nuno Espirito Santo kuondoka Wolves, klabu hiyo imemtangaza rasmi Bruno Lage kama kocha mkuu wa klabu hiyo kuanzia msimu ujao.
Lage alikuwa kocha wa Benfica ambapo alichukua nafasi ya Rui Vitoria mwezi Januari 2019. Akiwa Benfica, alifanikiwa kutwaa ubingwa wa ligi hiyo katika msimu wake wa kwanza. Hata hivyo mafanikio hayo hayakuwa na tija sana kwa Lage kwani aliondolewa klabuni hapo mwishoni mwa msimu uliopita.
Baada ya kukaa miezi 11 bila timu ya kuinoa, Lage ametua Molineux na sasa atakinoa kikosi cha Wolves ambacho kiliachana na Nuno kwa makubaliano maalumu ya pande zote zilizohusika.

Imeripotiwa kuwa, Nuno huenda akatua Crystal Palace japokuwa alishafanya majadiliano ya awali na Everton ikiwa ni miongoni mwa vilabu vinavyotafuta makocha wapya kuelea msimu ujao wa EPL.
Chukua namba yako ya akaunti na kiasi cha pesa unachotaka kuweka, sogea kwenye duka lolote la Meridianbet lililo karibu nawe utasaidiwa kuweka pesa.
Habari njema