Kiungo muhispania na mshindi wa Ballon d’Or 2024, Rodri, amesema kwa sasa akili yake yote ipo kwenye Kombe la Dunia na hataki kujadili chochote kuhusu mustakabali wake Manchester City hadi mashindano hayo yatakapomalizika. Nyota huyo mwenye miaka 29 amekuwa akihusishwa na tetesi za kuhamia Real Madrid huku mkataba wake ukiingia mwaka wa mwisho.

Rodri amekiri kuwa ni jambo la kawaida kwa majina ya klabu mbalimbali kutajwa pale mchezaji anapokaribia mwisho wa mkataba wake. Hata hivyo, amesisitiza kuwa hana presha yoyote kuhusu hali hiyo kwa sababu anafahamu vizuri nafasi yake na anataka kuielekeza nguvu zake zote katika kuiwakilisha Hispania kwenye jukwaa kubwa zaidi la soka duniani.
Hispania inaingia kwenye Kombe la Dunia ikiwa miongoni mwa timu zinazotajwa kuwania ubingwa, na Rodri anaamini mafanikio yatapatikana ikiwa wachezaji wataendelea kuwa wanyenyekevu. Mabingwa hao wa Ulaya watachuana na Cape Verde, Saudi Arabia na Uruguay katika Kundi H, huku wakitarajiwa kuonyesha kiwango cha juu kuanzia mchezo wao wa kwanza.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Nyota huyo wa Manchester City pia amefichua kuwa amewahamasisha wenzake kwa kutumia mfano wa gwiji wa tenisi Rafael Nadal. Baada ya kutazama filamu ya maisha ya Nadal, Rodri aliguswa na falsafa ya kupambana hadi mwisho bila kujiona bora kuliko wengine. Ameeleza kuwa mabingwa wakubwa hujengwa na juhudi za ziada, nidhamu na utayari wa kufanya kazi ngumu kila dakika ya mchezo.

Kwa sasa, mashabiki wa Manchester City na Real Madrid wataendelea kusubiri kuona uamuzi wake utakuwa upi baada ya Kombe la Dunia. Lakini Rodri anataka kwanza kuiongoza Hispania katika harakati za kutafuta taji la dunia kabla ya kufungua ukurasa mpya kuhusu maisha yake ya klabu.


