Nyota wa zamani wa klabu ya Barcelona na timu ya taifa ya Hispania, Xavi Iniesta amepinga vikali mpango wa klabu yake ya zamani ‘Barcelona’ kuwasajili wachezaji Pierre-Emerick Aubameyang na Sadio Mane.
Pierre-Emerick Aubameyang wa Arsenal na Sadio Mane wa Liverpool kama walikuwa na ndoto za kuchezea Barcelona katika maisha yao ya soka basi walifikirie vizuri wazo lao hilo.
Xavi Hernandez ambaye ni zao la shule ya michezo ya Barcelona ‘La masia’ anaamini kuwa Mane na Aunameyang hatoweza kumudu mtindo wa uchezaji soka wa Barcelona.
Xavi hana shida na uwezo wa wachezaji hao, lakini wasiwasi wake ni juu ya aina ya uchezaji wa wachezaji hao kumudu kuingia katika mfumo wa klabu ya Barcelona.
Mkataba wa Aubameyang na Arsenal unaelekea mwishoni kabisa na Aunameyang amegoma kabisa kusaini mkataba mpya na vigogo hao wa London pamoja na kuweka wazi ndoto zake za kuchezea ligi ya Hispania maarufu kama La Liga.
Kwa upande wa Sadio Mane yeye bado ana mkataba mrefu na Liverpool mpaka mwaka 2023 lakini kwa muda mrefu amekua akihusishwa na kuhitajika na kikosi cha Barcelona.
Ikumbukwe kwamba msimu wa 2018/19 ulikua msimu wa mafanikio makubwa kwa wote hawa wawili baada ya kumaliza wote kuibuka vinara wa ufungaji katika ligi kuu ya EPL. Wawili hao walishinda tuzo ya kiatu cha dhahabu pamoja na nyota mwingine wa mafarao wa Misri, Muhammed Sallah.
Wakati dunia inawatazama Aunameyang na Mane kama wachezaji hatari nanwenye uwezo wa hali ya juu wa kufunga, yeye Xavi anawatazama kama wenye uwezo wa kawaida tu na wanaweza kufunga pale tu ambapo kuna nafasi za wazi huku Barcelona ikihitaji wachezaji wawezao kutembea katika nafasi finyu na kuleta madhara kwa mpinzani.
Maoni haya ya Xavi yanaweza kupingwa na wadau wengi wa soka kwa sababu mbalimbali. Binafsi ninamuunga mkono kwa sababu kuu mbili;
Kwanza, Xavi anaijua vema Barcelona. Anajua ni nini inahitaji kwa wakati gani na nini haihitaji. Ikumbukee kuwa Xavi ni zao la shule ya vipajo ya Barcelona, La Masia na alijiunga hapo tangu akiwa na miaka 11! Amekua na Barcelona katika hali zote, amevuja jasho na damu kuiongoza Barcelona kushinda taji la La liga mara nane huku wakishinda ligi kuu ya mabingwa Ulaya ‘UEFA’ mara nne! Hivyo basi ni wazi kuwa Xavi anaijua vema falsafa ya soka la Barcelona ya ‘tik-tak’. Mfumo wa pasi fupifupi zikipigwa katika njia sahihi na timu ikicheza kama timu zaidi badala ya mchezaji mmoja mmoja kucheza katika nafasi yake tu.
Pili, Xavi hivi sasa ni kocha wa timu ya Al Sadd inayoshiriki ligi kuu ya Qatar.kwa hiyo ni wazi kuwa hatoi maoni ya kishabiki bali ya kitaalamu kama mwalimu wa soka.
Sababu hizo mbili zinatosha kabisa kumfanya mtu hata kama hakubaliani moja kwa moja na maoni ya Xavi basi angalau ayafikirie kwa mara ya pili.
SADICK
Ni maoni yake, sio kiongozi wa timu na uongozi wa sasa unaweza kuamua kinyume chake#Meridianbettz
Gabriel
Xavi yuko sahihi
David pere
Kwa maoni yake yeye kaona hawafai
Theonestina
Uongozi uyafanyie kazi maoni yake
Lombo
ayo n maoni yake
mathayo sonje
xavi kazeeka umri hadi akili, maana sio kwa kuwakataa hawa jamaa, hata kama mfumo ni mgeni kwao, ndio maana akawepo kocha kwa ajili hiyooo!!
Theckla
Asante kwa taarifa
aisha
Huo ni mtazamo wake
Devotha
Asante kwa taarifa
Rehema Dickson
Ayo ni maono yake ila wako vizuri uongozi ukiwaitaji uwachukue tu wako vizuri sana
Povel
Yupo sahh kwa utamaduni wa wakatalunya thnks meridian bet kwa information
Zeiyana iddi
Xavi yupo vizuri..!uwongozi uwangalie maamuzi yake
Evaluziga
Huo ni mtazamo wako
Shafii
Makala nimeipenda ngoja tusubili maamuzi ya management ya Barcelona
Antony Luseno
Xavi atakuwa na chembechembe za ubaguzi
Magdalena
Maoni yake nazuri
felister
uongozi ufanyie kazi maoni yake
Neema juma
Xavi yuko sahihi
winfrida
sisi mashabiki tunaona wako vizuri
Hamidu
Mtazomo wake! Mane ni Bora kwa sasa
Fundi wa mpira.#meridianbettz
Hamidu
Mtazamo wake!mane ni Bora kwa sasa fundi wa mpira# meridianbettz
Ernest
Ikumbukwe Lamasia siku hizi imekuwa haina vipaji vy akutisha lakini ukiwaangalia hawa jamaa ni wachezaji ambao wamekuwa wakisumbua ulimwengu wa soka kwa sasa!!! Hapa Xavi kapuyanga
mwakalosi
sasa mane na pierre inabidi wakathibitishe kuwa xavi kakosea kuwa kana
frank patrick
Ni kweli hawaendani na aina ya mpira unaopigwa barca …NAUNGANA NA KAULI YA FUNDI XAVI
Genia Sikaluzwe
Good news