Klabu ya soka ya Yanga SC, wametwaa ubingwa wa ligi kuu Tanzania bara, kufuatia ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Coastal Union jana Jumatano kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa, jijini Dar es salaam.
Mabao ya Yanga yaliwekwa wavuni na washambuliaji wake Wakongo, Fiston Kalala Mayele, mawili dakika ya 35 na 68 na Chico Ushindi Wakubanza dakika ya 52.
Kwa ushindi huo, Yanga SC inafikisha alama 67 katika michezo wa 27, alama ambazo hakuna timu inayoweza kufikisha wakiwa wamesalia na michezo 3 mkononi.
Yanga SC wametwaa ubingwa huo baada ya miaka 4 ambayo imekuwa katika utawala wa watani wao wa jadi Simba SC ambao wanakamata nafasi ya nne katika msimamo wa ligi.
ALIYA’S WISHES
Bila shaka unatamani ushindi mkubwa, vipi kuhusu kujaribu Sloti hii ya Aliya’s Wishes? jaribu ushinde sasa.