Yanga ikiwa Uwanja wa Mkapa imegawana pointi mojamoja na Namungo FC ya Lindi kwenye mchezo wa ligi raundi ya 11.
Bigirimana Blaise, leo Novemba 22 amemwaga machozi baada ya dakika 90 kukamilika kutokana na kitendo cha kukosa penalti dakika ya 90 baada ya kipa namba moja wa Yanga kuiokoa kwa kuitema na aliporudia mara ya pili alipaisha mpira huo mazima.
Yanga ikiwa Uwanja wa Mkapa imelazimisha sare ya kufungana bao 1-1 dhidi ya Namungo kwenye mchezo uliokuwa na ushindani mkubwa mwanzo mwisho.
Mabao ya timu zote mbili yalipatikana kipindi cha kwanza ambapo Carlos Carlinhos alifunga bao la kwanza kwa Yanga dakika ya 13 kwa pasi ya Kibwana Shomari na dakika ya 16, Stephen Sey alipachika bao la kusawazisha kwa guu la kushoto.

Penalti ya Blaise iliyopaishwa ilipatikana dakika ya 90 baada ya beki,Bakari Mwamnyeto kumchezea faulo kiungo Shiza Kichuya ndani ya 18 na alionyeshwa kadi ya njano.
Mvutano mkubwa ilikuwa ni nani ambaye angepiga penalti hiyo jukumu likawa la Blaise mwenye mabao manne ambaye alikosa penalti hiyo baada ya Mnata kumsoma kwa umakini na kuipangua jumlajumla.

Sare hiyo inaifanya Yanga kugawana pointi mojamoja na Namungo FC Uwanja wa Mkapa huku Mnata akipewa zawadi ya noti na mashabiki baada ya kutimiza majukumu yake kwa umakini.
Yanga inafikisha jumla ya pointi 25 sawa na Azam FC ambayo ipo kileleni kwa idadi ya mabao huku Namungo ikibaki nafasi ya 9 na pointi zake ni 15.
Hadi 130,000,000 TSH Kutolewa kwa washiriki wa shindano la Playson Cashfall. Unaipata kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet Pekee. Jisajili sasa, kisha ingia mchezoni kabla ya Novemba 29.




Adelta
Mechi ilikuwa si ya kitoto
Mwajumah
Yanga hawana jipya hao wamenusurika kidogo tu wangeipata habari yao ila Namongo walijua kunifurahisha jmn
Shakila mrope
Hawo yanga hamna kitu ni utopolo tu
Angelina
Utopolo kama utopolo
Fatina mfingi
Yanga jan bahat yao mbon lingewakut jambo
Ester jackson
Kwa jirani zetu wanafurahi kweli jamani kwa mchezo wa Jana yanga waliucheza vilivyo kwenye kiwango bora kwanza walioata nafasi nyingi za kufunga ingawa haikuwa bahati kwao yanga iliyo pita sio ya sasa tukumbuke hasaivi ndiyo tunaionea raha yanga timu ya namungu ilikuwa ni kawaida tu kuifunga yanga lakini hasaivi tunaona inaboreka yaka ila kwa wasio jua mpira wanaongea hatari tunatakiwa kuiangalia yanga iliyopita na hasaivi ndio muongee nyinyi wa porini
Elika
Safi sana namungo maana mashabiki wa yanga mnaongea sana..niliipenda kwakweli ile droo kwenye mechi ya yanga na namungo
Tatu
Yanga wamejitahidi
magdalena
namungo walijitahidi sana ila yanga walibebwa sana
Lydia Emmanuel Magoti
Hii mechi ilikuwa yakuvutana mashati vuta nikuvute namongo walikuwa moto Sana isingekuwa ilepenati tungeongea mengine
Salma ngende
Mhii
Fatuma kasomo
Yanga ilibakia kidogo wakalishwe
Mariam mtandama
Safi
Antony Luseno
Kwa sare hii ni shangwe kwa timu pinzani
Sania
Namungo wanajitahidi sana
Sarah
Wamejitahidi sana yanga
Rahma
Safi
Hopemwaikuka
🤣🤣🤣
Povel
Habar mbaya kwa mashabik wa yanga ila kwa upande wa pili wanashukuru kwa kupunguzah gape la point na watani wao
aisha
Yanga timu mbovu
Saupha mohamed
Yanga hawana kaziii
Tahiya
Namungo jeshi
Issa
Namungo wamejitahid kutoa suluhu a mabingewa
Sauda
Bonge la mechi
Janeflora malisa
😂😂😂
warda
Nilijua tu watakaa