Yanga Yasuluhu na JKT Tanzania, Vurugu Zilitawala

Patrick Sibomana, mshambuliaji wa Yanga, jana alipindua meza kibabe kwa kufunga bao la kusawazisha mbele ya JKT Tanzania kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa Uwanja wa Jamhuri, Dodoma.

Mchezo huo ulikamilika kwaYanga kufungana na JKT Tanzania, bao 1-1 na kugawana pointi mojamoja, makao makuu ya nchi ya Tanzania, Dodoma. Licha ya Michael Aidan wa JKT Tanzania kufunga bao akiwa nje ya 18 kwa kuachia shuti kali dakika ya 13 halikuwapa pointi tatu JKT Tanzania.

Kuingia kwa Sibomana kulibadilisha mchezo jumla kwa kutuliza timu baada ya kunyanyuliwa benchi na Kocha Mkuu, Luc Eymael dakika ya 52 akichukua nafasi ya kiungo mshambuliaji Mapinduzi Balama.

Bao la Yanga lilipatikana baada ya kiungo mshambuliaji wa Yanga, Haruna Niyonzima  kuachia shuti kali langoni mwa JKT Tanzania lililotemwa na mlinda mlango wa JKT Tanzania ndipo likakutana na guu la Sibomana aliyeujaza moja kwa moja langoni.

Ushindi huo unaifanya Yanga ikusanye jumla ya pointi nne kwa JKT Tanzania msimu huu na mabao manne kwani kwenye mchezo wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Uhuru, Yanga ilishinda mabao 3-2.

Beki Lamine Moro wa Yanga alionyeshwa kadi nyekundu dakika ya 88 kwa kumchezea mchezo usio wa kiuungwana Mwinyi Kazimoto wa JKT Tanzania ambaye naye pia alionyeshwa kadi nyekundu.

36 Komentara

    Hii mechi ilikuwa na vurugu sana walikamiana sana

    Jibu

    Alichokifany beki lamine Moro co fair play kabisa kwn hata FIFA wasisitizah wanamichezo kupendana kwa kitendo kile sheria ifuate mkondo wake iwe funzo kwa wavunja sheria wengne thnks meridian bet tz kwa information

    Jibu

    Mchezo wajana hauku nifurahisha kabisa mana walikuwa wanapigana mitama bila ya kucheza katika nafasi yake

    Jibu

    Nilikuwa natamani yanga wafugwe

    Jibu

    Yanga apunguze kujiamini wanawapoteza mashabiki wake

    Jibu

    Yanga wazee wavurugu

    Jibu

    Yanga wapunguze vurugu

    Jibu

    Mechi ilikuwa sio poa yanga walishikwa atarii vurugu mtindo moja

    Jibu

    Yangaa wanacheza kwa fujo Sana

    Jibu

    Corona imewaathili yanga,lakini kwa upande wa jkt wale ni wajeda muda wote wapo na tizi Kama kawaida

    Jibu

    Hii mechi ilikuwa na vurugu sana

    Jibu

    Sawa sio mbaya

    Jibu

    hawa utopolo wao ni suluhu tu labda wanaweza kuifunga arsenal tu

    Jibu

    Yanga hawana lolote vurugu nyingitu

    Jibu

    Simba wapewe ubingwa tu akuna jins# meridianbettz

    Jibu

    Daaa haikuwa poa

    Jibu

    Yanga ya sasa sio ile yanga ya zamani..yanga wako vibaya sana inatakiwa wafanye na mabadiliko kidogo…kiukweli yanga hawajielewi

    Jibu

    Yanga sijui Wana tatzo gani takribani mechi nyingi wanatoka sare wanabidi wabadilike

    Jibu

    Yanga wanatoa sare sare

    Jibu

    JKT msimu huu imepania sana vilabu vikongowe asa simba na yanga

    Jibu

    Maoni:#meridianbettz asante kwa taarifa

    Jibu

    Kitendo cha Lamine Moro kimemuondoa kwenye mchezo wa kiungwana na sikuona sababu ambayo ingeweza kumusukuma kufanya vile#meridianbettz

    Jibu

    Mmh haikuleta picha nzuri hiyo

    Jibu

    Hii mechi kila timu ikiikamia ndio maana kukatokea vurugu nyingi sana

    Jibu

    Yanga bhana wanazidi tu kujishusha hazi wanan,gan,gania msemo wao yanga ya wanachi

    Jibu

    Haikua mechi nzuri

    Jibu

    safi sana yanga

    Jibu

    Safi sana yanga

    Jibu

    Lamine moro hakufanya uungwana na kufanya game iwe na vurugu

    Jibu

    Huyu Lamine ameona jina lake halitajwi tajwi ndo kaona atafute kiki#Meridianbettz

    Jibu

    Yanga hamana kitu.

    Jibu

    Yanga ilikuwa inanafas nzur ya ushindi

    Jibu

    Siwaelewag hao

    Jibu

    Kusema kwel bwana soka la kibongo linaumiza sana mioyo ya watu mnoo hakuna uhakika wa mechi sisi Tanzania bado sana hasa wanao umia zaid mashabiki wa timu fulan ndio mm binafsi bora niwe uingereza tuu soka la bongo linaumiza sana hisia za watu bora nisiwe mzalendoo tuu wa kuacha.kushabikia nyumban lakn nipate ile burudan nayo itaka

    Jibu

    Hahaha haya motokeo tuliyategemea kabisa maana wote hawakujipanga

    Jibu

    Mechi ilikua na vurugu had kero

    Jibu

Acha ujumbe