Zidane Ana Mpango wa Kurejea Italia?

Kocha wa Real Madrid Zinedine Zidane alisema Italia ‘wakati wote imekuwa moyoni mwangu’ na alisisitiza Juventus ‘imekuwa muhimu kwangu kila wakati.”

Kocha huyo Mfaransa alizungumza na Sky Sport Italia baada ya Real Madrid kushinda 3-1 dhidi ya Liverpool Jumanne, wakati Real wakijihakikishia nafuu kuelekea mchezo wa marudiano katika robo fainali ya Ligi ya Mabingwa.

Zidane alifurahi na ushindi lakini alisisitiza wababe hao wa La Liga bado wanapaswa kumaliza kazi hiyo.

Akizungumzia ushindi alisema kuwa licha ya kupata ushindi, wanahitaji kutambua kuwa kuna mechi ya marudiano, na wanahitaji kumaliza kazi waliyoianza.

Zinedine Zidane
Kumbukizi: Zidane akiwa Juventus

“Lakini narudia, tunaweza kufurahi na mechi usiku wa leo, kwa sababu tulicheza mchezo kamili.”

Mshindi huyu wa Kombe la Dunia aliulizwa ikiwa inawezekana kumuona akirejea kwenye soka la Italia, na Zidane alisema bado ana uhusiano wa kipekee na Bianconeri, ambapo alikaa miaka mitano kama mchezaji kati ya 1996 na 2001.

“Italia daima iko moyoni mwangu. Juventus daima imekuwa muhimu kwangu, Sijui [kama nitarejea tena Italia]. Sasa niko hapa. Hebu tuone.”


 

INAWEZEKANA KUWA MILIONEA BILA KUVUJA JASHO NA KASINO YA ODD ONE OUT.

Odd One Out kutoka Meridianbet ni moja ya kasino maridhawa yenye picha halisi, ambayo inakupa nafasi ya kushinda kadri uwezavyo na kuwa milionea mara baada ya mzunguko kukamilika.

CHEZA HAPA

4 Komentara

    Bora aende Italy mana wanamzingua tu

    Jibu

    Zidane jina kubwa

    Jibu

    Zidane Yuko vizuri

    Jibu

    Vzur

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.