Mchezaji mkongwe wa Ac Milan, Zlatan Ibrahimovic amejikuta kwenye hatia na kupigwa faini ya Euro 50,000 baada ya kubainika kuwa alikuwa na hisa kwenye kampuni ya kamari.

Baada ya uchunguzi uliofanywa na UEFA imebainika kuwa mchezaji huyo wa Serie A anamiliki asilimia 10 ya hisa katika kampuni ya kamari ya Berthard, hivyo kosa hilo linavunja moja kwa moja sheria za kinidhamu za UEFA.

Yaliyosemwa na UEFA,

Mwenyekiti wa UEFA ameamua kumpiga faini ya Euro 50,000 kwa Zlatan Ibrahimovic kwa kuvunja kifungu namba 12(2)b cha kitengo cha nidhamu yaani kuwa uhusiano wa kifedha na kampuni ya kubashiri”

“Mwenyekiti wa UEFA inaamuru pia bwana Ibrahimovic ajiondoe kwenye ushiriki wa kampuni tajwa. Mwisho, mwenyekiti ameamua kuionya AC Milan na kupiga faini ya euro 25,000 kwa kuruhusu kuwa na mchezaji anayejihusisha na kumiliki hisa katika kampuni ya kubashiri.

UEFA imetoa maamuzi makubwa sana hapo jana na Zlatan ni mmoja tu ya watu waliokumbwa na adhabu kutoka kwenye shirikisho hili la soka ulaya, kwingineko ni kuhusu lile sakata la European Supper League ambapo Barcelona, Madrid na Juventus wameingizwa matatani baada ya kukataa kujitoa.


BONASI YA 50% KILA SIKU KATIKA KASINO ZA EVOPLAY HAPA MERIDIANBET.

Meridianbet na Evoplay Kasino wanakupa bonasi ya 50% ya kiasi utakachoweka katika akaunti yako leo. Unasubiri nini ni wakati wa kupiga pesa sasa na Mabingwa.

tuchel, Tuchel :Tuna Bahati Tottenham Wametusaidia Kazi., Meridianbet

SOMA ZAIDI

2 MAONI

JIBU

Tafadhali andika maoni yako
Tafadhali andika jina lako hapa