Nyota wa zamani wa soka duniani David Beckham amefichua kile anachoamini kuwa kimeifanya mbinu za kocha Luis Enrique kufanikiwa ndani ya Paris Saint-Germain, baada ya klabu hiyo kufuzu fainali ya UEFA Champions League kwa mara ya pili ndani ya miaka miwili.
Beckham alisema baada ya PSG kutoka sare ya 1-1 dhidi ya Bayern Munich, kuwa Enrique ameijenga timu yenye mshikamano mkubwa na nidhamu ya hali ya juu, jambo ambalo limeifanya PSG kuwa na ubora mkubwa msimu huu.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Akiwapongeza vijana wa PSG, Beckham alisema “Ni timu changa lakini yenye umoja mkubwa sana. Enrique amewajenga kuwa wachezaji wanaoelewana na kushirikiana kwa kila hali.”
Beckham pia alifichua kile alichosema kutoka kwa rais wa PSG kuhusu kocha huyo. “Rais wa PSG, Nasser Al-Khelaifi, alisema kuwa katika mwaka wake wa kwanza, Luis Enrique karibu kila siku alikuwa analala kwenye kituo cha mazoezi,” alisema Beckham.
Aliendelea kueleza kujitoa kwa Enrique katika kazi yake ya ujenzi wa timu, akisema “Alikuwa akifanya kazi ya kuamua jinsi timu itacheza, nani anahitajika, na mustakabali wa timu unapaswa kuwa vipi.”
Beckham alihitimisha kwa kusema Enrique ameunda kikosi chenye nidhamu na malengo ya pamoja. “Anataka wachezaji wote wafanye kazi kwa kiwango sawa, wawe na nia moja. Anawajenga vijana na anataka wachezaji wanaokimbia na wasiosimama. Hicho ndicho alichokijenga,” alisisitiza. PSG kwa sasa wanaongoza Ligue 1 kwa pointi sita na wanajiandaa kucheza fainali ya Champions League dhidi ya Arsenal mjini Budapest Mei 30.


