Enrique Apuuza Kauli Ya Arteta Kabla Ya Fainali

Kocha wa PSG, Luis Enrique, amesema hana shaka na uwezo wa Arsenal baada ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu England, akimpongeza Mikel Arteta kwa kazi kubwa aliyoifanya tangu alipochukua mikoba ya kuinoa klabu hiyo.

Enrique Apuuza Kauli Ya Arteta Kabla Ya FainaliAkizungumza kuelekea fainali ya UEFA Champions League, Enrique alisema Arsenal na PSG zinafanana kwa namna nyingi licha ya kila timu kuwa na njia yake ya kufikia mafanikio ya msimu huu.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Kocha huyo wa Hispania alieleza kuwa PSG imefanya maandalizi ya kina kwa kuichambua Arsenal, timu ambayo wamekutana nayo mara kadhaa katika misimu ya hivi karibuni, huku akisisitiza kuwa fainali ni mchezo tofauti na mingine yote.

Enrique Apuuza Kauli Ya Arteta Kabla Ya Fainali
Enrique pia alikataa kuipa timu yoyote nafasi ya kuwa favorit katika mchezo huo, akisisitiza kuwa mafanikio yatategemea umakini na utekelezaji wa mipango ndani ya dakika 90 za mchezo.

“Sioni kama kuna timu iliyo mbele ya nyingine. Arsenal na sisi tunalenga kitu kimoja, lakini tumefika hapa kupitia njia tofauti. Fainali huwa ngumu kila wakati, hivyo tutapaswa kutoa kila kitu tulichonacho huku tukifurahia mchezo huo,” alisema Enrique.

Enrique Apuuza Kauli Ya Arteta Kabla Ya Fainali

Akizungumzia kauli ya Arteta aliyesema Arsenal itakuwa mabingwa wa Ulaya, Enrique alisema PSG haihitaji motisha ya ziada kwani nafasi ya kushinda Champions League pekee inatosha kuwapa hamasa kubwa ya kupambana na kutetea heshima yao katika soka la Ulaya.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.