Kocha wa Bayern Munich, Vincent Kompany, amesema timu yake inajipanga kufanya tukio lisilosahaulika wakati watakapokutana na Paris Saint-Germain katika mchezo wa mkondo wa pili wa nusu fainali ya UEFA Champions League.
Bayern wanakabiliwa na kazi kubwa baada ya kupoteza mchezo wa kwanza kwa mabao 5-4, lakini Kompany amesema kikosi chake kimejaa imani kubwa. Alisema “Kuna hisia kwamba pamoja tunaweza kuchukua hatua inayofuata. Wachezaji na mashabiki wanaamini tunaweza kufika fainali.”
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Kocha huyo aliongeza kuwa Bayern wamepiga hatua kubwa msimu huu, akisema “Ni wachache waliamini mwanzoni mwa msimu kwamba tutakuwa na nafasi ya kufika hatua hii, lakini sasa tupo hapa na tunapambana hadi mwisho.”
Pia alisisitiza utulivu ndani ya kikosi chake licha ya presha ya mchezo mkubwa, akisema “Utulivu wa hali ya juu, ndani ya timu kuna utulivu. Hatutaki mchezo huu ututawale mapema kichwani.”
Kompany alieleza kuwa maandalizi yao yanalenga maamuzi madogo yatakayosaidia kupata ushindi, akisema “Tunatafuta asilimia hiyo ya mwisho itakayotupa ushindi. Kipaumbele chetu ni kushinda mchezo.”
Bayern tayari wameshinda taji la Bundesliga msimu huu na bado wana nafasi ya kutwaa mataji mawili, lakini macho yote sasa yameelekezwa kwenye mchezo huu muhimu wa Ulaya utakaofanyika nyumbani dhidi ya PSG.


