Kocha Luis Enrique ameweka wazi mtazamo wake kuelekea fainali ya UEFA Champions League, ambapo Paris Saint-Germain itavaana na Arsenal. Enrique amesema licha ya kuheshimu uwezo wa Arsenal, hakuwa na hofu kubwa nao kama ilivyokuwa kwa Bayern Munich.
Akizungumza na waandishi wa habari, Enrique alisema “Kama kuna timu niliyoogopa, ilikuwa FC Bayern Munich. Arsenal wamekuwa imara hivi karibuni, lakini kusema kweli, sijawahi kuwawazia sana.” Kauli hiyo imezua mjadala mkubwa miongoni mwa mashabiki kuelekea mchezo huo mkubwa wa fainali.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
PSG ilitinga fainali baada ya kuiondoa Bayern Munich kwa jumla ya mabao 6-5. Katika mchezo wa mkondo wa pili uliopigwa Mei 6, 2026, timu hizo zilitoka sare ya 1-1 kwenye uwanja wa Allianz Arena, matokeo yaliyowapeleka PSG mbele kutokana na ushindi wa 5-4 walioupata Paris kwenye mkondo wa kwanza.
Kwa upande wa Arsenal, timu hiyo ilifuzu fainali baada ya kuiondoa Atlético Madrid kwa jumla ya mabao 2-1. Ushindi wa 1-0 kwenye uwanja wa Emirates kupitia bao la Bukayo Saka dakika ya 44 uliihakikishia nafasi ya kucheza fainali, baada ya sare ya 1-1 katika mchezo wa kwanza Madrid.
Enrique pia alisisitiza kuwa PSG haitaingia uwanjani kwa mbinu za kujilinda. “Hatutakwenda kujilinda. Tunajua fainali inahitaji ujasiri na ubunifu. Tutacheza mpira wetu,” aliongeza kocha huyo.
Fainali hiyo ya UEFA Champions League inatarajiwa kuwa ya ushindani mkali kati ya timu mbili zenye uwezo mkubwa msimu huu, huku macho ya mashabiki duniani yakiwaelekea PSG na Arsenal katika pambano la kuwania ubingwa wa Ulaya.


