Manchester United Wamuwania Ederson Kuchukua Nafasi ya Casemiro

Klabu ya Manchester United imeanza rasmi maandalizi ya kuziba pengo litakaloachwa na kiungo wao tegemeo Casemiro, ambaye anatarajiwa kuondoka mwishoni mwa msimu huu wa kiangazi. Baada ya kuitumikia timu hiyo kwa miaka minne, nyota huyo wa Brazil alithibitisha Januari kuwa huu utakuwa msimu wake wa mwisho ndani ya dimba la Old Trafford.

Manchester United Wamuwania Ederson Kuchukua Nafasi ya CasemiroKatika kipindi chake cha mwisho, Casemiro amekuwa na mchango mkubwa, hasa tangu Michael Carrick alipochukua jukumu la kuinoa timu mwezi Januari. Kiungo huyo ameonyesha ubora wake kwa kufunga mabao matano katika mechi 12 za hivi karibuni za Ligi Kuu England, huku akiendelea kuwa mhimili katika eneo la kiungo kwa kazi ya ukabaji na kusaidia mashambulizi.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Kutokana na umuhimu wake, Manchester United wanajua wazi kuwa ni lazima wapate mbadala mwenye ubora sawa au zaidi. Jicho lao limeelekezwa kwa kiungo wa Atalanta, Ederson, ambaye ameonyesha uwezo mkubwa katika Serie A msimu huu.

Manchester United Wamuwania Ederson Kuchukua Nafasi ya CasemiroKwa mujibu wa taarifa, Atalanta wanahitaji ada ya pauni milioni 39 kwa ajili ya kumuuza nyota huyo, ingawa kuna matumaini kuwa dau hilo linaweza kupunguzwa kutokana na mkataba wake unaomalizika mwaka 2027. Manchester United wameonyesha nia ya dhati kwa kumtengea ofa ya mshahara wa euro milioni 4.5 kwa mwaka, sawa na takribani pauni 75,000 kwa wiki.

Manchester United Wamuwania Ederson Kuchukua Nafasi ya CasemiroAkizungumza kupitia kituo cha YouTube cha Fabrizio Romano, mwandishi wa habari za usajili Matteo Moretto alisema “Manchester United wako tayari kumpa Ederson mshahara wa euro milioni 4.5 kwa mwaka. Arsenal pia wameonyesha nia, lakini United wameizidi Atletico Madrid kwa ofa yao.”

Manchester United Wamuwania Ederson Kuchukua Nafasi ya CasemiroAliongeza “Hadi sasa hakuna klabu iliyofikia makubaliano rasmi na Atalanta, lakini Manchester United wana nafasi kubwa kifedha kuliko wengine katika kukamilisha dili hilo.” Ederson, ambaye ni kiungo mwenye nguvu na uwezo wa ukabaji kama Casemiro, amecheza mechi 39 katika mashindano yote msimu huu na kufunga mabao mawili, akionekana kuwa chaguo sahihi kuchukua nafasi ya mkongwe huyo wa Brazil.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.