Klabu za Paris Saint-Germain na Manchester United zinatajwa kuwania saini ya kiungo wa West Ham United, Mateus Fernandes, huku klabu hiyo ikijiandaa kumuzaa nyota huyo katika dirisha lijalo la usajili.
West Ham ipo kwenye hatari ya kushuka daraja baada ya kubakiwa na michezo miwili ya mwisho ya msimu wakihitaji kufuta tofauti ya pointi mbili dhidi ya Tottenham Hotspur ili kujinusuru kutoka eneo la kushuka daraja.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Katika mchezo wao ujao, West Ham watasafiri kuwavaa Newcastle United kabla ya kuikaribisha Leeds United kwenye mchezo wa mwisho wa msimu. Endapo watapoteza dhidi ya Newcastle na Tottenham wakaifunga Chelsea FC, basi kushuka kwao kwenda Championship kunaweza kuthibitishwa mapema.
Ripoti kutoka The Athletic zimeeleza kuwa viongozi wa West Ham tayari “wanajiandaa kuishi bila Fernandes”, huku wakipanga kumuuza ili kupata fedha za usajili wa wachezaji wapya, bila kujali watabaki Ligi Kuu au watashuka daraja.
Fernandes mwenye umri wa miaka 21 ameonyesha kiwango bora tangu aliposajiliwa akitokea Southampton FC majira ya kiangazi yaliyopita. Kiungo huyo ameongeza mchango mkubwa baada ya kuondoka kwa Lucas Paqueta, akihusika kwenye mabao tisa katika michezo 40 msimu huu.
“Paris Saint-Germain na Manchester United zinafuatilia kwa karibu maendeleo ya Fernandes huku thamani yake ikipewa nafasi ya kuongezeka zaidi iwapo atafanya vizuri kwenye Kombe la Dunia akiwa na Ureno,” ilieleza sehemu ya ripoti hiyo.



