Bondia muingereza Amir Khan ameibuka na kumuonya bondia mwenzake Conor Benn kuhusu pambano lake na Samuel Vargas jioni ya leo.
Amir Khan amemwambia Benn kuwa makini akiwa anapigana na bondia huyo Samuel Vargaz kuwa ni mtu mwenye ujuzi mkubwa wa kupambana. Wakati wa pambano la Khan na Samuel, Khan alishinda lakini alipigika sana. Hivyo ni mtu sahihi kutoa ushauri kwa Benn.
“Itabidi uwe makini katika pambano hili, hii ni ndondi na ngumi moja tu inaweza kuamua nani mshindi.” Alisema Khan.
Kwa upande wa pili Benn amesema kuwa analitambua hilo na yupo tayari kupambana na bondia huyo. Aeleza kuwa ametazama marejeo ya video nyingi za mapambano ya Samuel na anaamini kuwa ni mpiganaji mzuri na yeye amejiandaa kwa hilo.
Wakati dunia ikiwa inajiandaa kutazama pambano kati ya Amir Khan na Kell Brooks, Benn aeleza kuwa wawili hao ndio watu wawili wanaompa moyo sana kwenye kazi yake na anatamani kupigana na mmoja wao.
INAWEZEKANA KUWA MILIONEA BILA KUVUJA JASHO NA KASINO YA ODD ONE OUT.
Odd One Out kutoka Meridianbet ni moja ya kasino maridhawa yenye picha halisi, ambayo inakupa nafasi ya kushinda kadri uwezavyo na kuwa milionea mara baada ya mzunguko kukamilika.
CHEZA HAPA
Adelta
Ngoja tuone itakuwaje
Sarah
Tunasubiri tuone
neema juma
Bongee la pambano
warda
Haya tena yetu macho
Hopemwaikuka
Gud