Kocha Mkuu wa timu ya taifa ya Ivory Coast, Emerse Faé ametangaza kikosi cha wachezaji watakaoiwakilisha nchi hiyo kwenye michuano ya Kombe la Dunia 2026 kinachotarajiwa kuanza mwezi ujao.
Kikosi hicho kimejumuisha mastaa kadhaa wanaocheza katika ligi kubwa barani Ulaya, huku safu ya kiungo na ushambuliaji ikionekana kuwa na nguvu kubwa kutokana na uwepo wa majina makubwa yenye uzoefu wa kimataifa.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Miongoni mwa wachezaji waliotajwa kwenye kikosi hicho ni Franck Kessié, Seko Fofana, Simon Adingra pamoja na Nicolas Pépé ambao wanatarajiwa kuwa tegemeo kubwa katika mashindano hayo.
“Tumewaita wachezaji ambao wana uwezo, uzoefu na ushindani mkubwa wa kimataifa ili kuhakikisha tunakuwa na kikosi imara kwa ajili ya michuano hii,” alisema Emerse Faé wakati akitangaza majina ya kikosi hicho.
Katika kikosi hicho, makipa walioitwa ni Yahia Fofana, Mohamed Koné na Alban Lafont, huku safu ya ulinzi ikiongozwa na majina kama Ousmane Diomandé, Evan Ndicka na Wilfried Singo, wakati eneo la ushambuliaji likiwa na mastaa hatari akiwemo Amad Diallo na Elye Wahi.


