Neymar Ajumuishwa Kikosi cha Brazil Kombe la Dunia 2026

Neymar ametajwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Brazil kitakachoshiriki Kombe la Dunia 2026, huku mshambuliaji wa Chelsea F.C. Joao Pedro na winga wa Real Betis Antony wakikosa nafasi kwenye kikosi hicho.

Neymar Ajumuishwa Kikosi cha Brazil Kombe la Dunia 2026Kocha wa Brazil Carlo Ancelotti alitangaza kikosi hicho Jumatatu katika hafla iliyofanyika kwenye Makumbusho ya Tomorrow mjini Rio de Janeiro, huku waandishi wengi wa habari na mashabiki wakisubiri kwa hamu uamuzi wake kuhusu Neymar.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Nyota huyo mwenye umri wa miaka 34 anarudi kwenye kikosi cha Brazil baada ya kukaa nje kwa muda mrefu kutokana na majeraha yaliyomuondoa kwenye michezo mingi ya hatua za kufuzu Kombe la Dunia. Neymar ambaye ndiye mfungaji bora wa muda wote wa Brazil akiwa na mabao 79, hajacheza kwa timu ya taifa tangu mwaka 2023.

Neymar Ajumuishwa Kikosi cha Brazil Kombe la Dunia 2026Akizungumza na waandishi wa habari, Ancelotti alisema uamuzi wa kumjumuisha Neymar umetokana na kiwango chake cha sasa pamoja na utimamu wake wa mwili.

“Tumemfuatilia Neymar kwa mwaka mzima na tumeona hivi karibuni amecheza mara kwa mara huku akiwa ameimarika kimwili. Ana majukumu sawa na wachezaji wengine lakini uzoefu wake ni muhimu kwa timu,” alisema Ancelotti.

Neymar Ajumuishwa Kikosi cha Brazil Kombe la Dunia 2026Kwa upande wake Neymar alisema ameridhishwa na kiwango chake cha sasa licha ya changamoto za majeraha alizopitia akiwa Al Hilal SFC kabla ya kurejea Santos FC.

Neymar Ajumuishwa Kikosi cha Brazil Kombe la Dunia 2026
“Kimwili najisikia vizuri sana. Nimekuwa nikiboreka katika kila mchezo,” alisema Neymar baada ya Santos kupoteza mabao 3-0 dhidi ya Coritiba.

Neymar Ajumuishwa Kikosi cha Brazil Kombe la Dunia 2026Majina mengine makubwa yaliyojumuishwa kwenye kikosi hicho ni Vinicius Junior, Raphinha, Matheus Cunha na Endrick. Hata hivyo, Rodrygo, Eder Militao pamoja na Estevao wamekosekana kutokana na majeraha.

Neymar Ajumuishwa Kikosi cha Brazil Kombe la Dunia 2026Brazil itaanza kampeni yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo dhidi ya Morocco Juni 13 mjini New Jersey kabla ya kucheza dhidi ya Haiti na Scotland katika Kundi C.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.