Neymar ametajwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Brazil kitakachoshiriki Kombe la Dunia 2026, huku mshambuliaji wa Chelsea F.C. Joao Pedro na winga wa Real Betis Antony wakikosa nafasi kwenye kikosi hicho.
Kocha wa Brazil Carlo Ancelotti alitangaza kikosi hicho Jumatatu katika hafla iliyofanyika kwenye Makumbusho ya Tomorrow mjini Rio de Janeiro, huku waandishi wengi wa habari na mashabiki wakisubiri kwa hamu uamuzi wake kuhusu Neymar.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 34 anarudi kwenye kikosi cha Brazil baada ya kukaa nje kwa muda mrefu kutokana na majeraha yaliyomuondoa kwenye michezo mingi ya hatua za kufuzu Kombe la Dunia. Neymar ambaye ndiye mfungaji bora wa muda wote wa Brazil akiwa na mabao 79, hajacheza kwa timu ya taifa tangu mwaka 2023.
Akizungumza na waandishi wa habari, Ancelotti alisema uamuzi wa kumjumuisha Neymar umetokana na kiwango chake cha sasa pamoja na utimamu wake wa mwili.
“Tumemfuatilia Neymar kwa mwaka mzima na tumeona hivi karibuni amecheza mara kwa mara huku akiwa ameimarika kimwili. Ana majukumu sawa na wachezaji wengine lakini uzoefu wake ni muhimu kwa timu,” alisema Ancelotti.
Kwa upande wake Neymar alisema ameridhishwa na kiwango chake cha sasa licha ya changamoto za majeraha alizopitia akiwa Al Hilal SFC kabla ya kurejea Santos FC.

Majina mengine makubwa yaliyojumuishwa kwenye kikosi hicho ni Vinicius Junior, Raphinha, Matheus Cunha na Endrick. Hata hivyo, Rodrygo, Eder Militao pamoja na Estevao wamekosekana kutokana na majeraha.
Brazil itaanza kampeni yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo dhidi ya Morocco Juni 13 mjini New Jersey kabla ya kucheza dhidi ya Haiti na Scotland katika Kundi C.


