Garcia: Mchanganyiko wa Vijana na Wakongwe Unaweza Kutupatia Kombe

Beki wa FC Barcelona na timu ya Taifa ya Uhispania Eric Garcia anaamini kuwa mchanganyiko wa kuvutia wa Uhispania wa vijana wenye vipaji na wakongwe wenye uzoefu unaweza kuwaona wakiishinda timu yoyote kwenye Kombe la Dunia nchini Qatar.

Kati ya 2008 na 2012, Uhispania ilinyanyua mataji mawili ya Ubingwa wa Ulaya na pia kushinda Kombe lao la kwanza la Dunia huku wakitawala soka la Kimataifa, wakijivunia nyota kama vile Andres Iniesta, Iker Casillas na David Villa.

Hata hivyo, tangu ushindi huo wa Euro 2012, Hispania haijafanikiwa kurejea kwenye fainali ya michuano hiyo mikubwa na wachezaji wengi wao wakubwa kutoka miaka hiyo ya mataji wamestaafu.gARCIASergio Busquets na Jordi Alba pekee ndio waliosalia kutoka kwenye kikosi hicho cha Euro 2012, lakini kuibuka kwa vijana wenye vipaji vya kusisimua kama vile Ansu Fati na Pedri kumefufua matumaini ya kufanikiwa kurejea chini ya usimamizi wa Luis Enrique.

Garcia anahisi mchanganyiko wa Uhispania wa wakongwe na vijana wenye vipaji, kama vile Busquets na Alba, ukiongeza na mbwembwe zao za kusisimua zinaweza kusababisha mchuano mzuri nchini Qatar.

Garcia aliiambia SPORT; “Kwangu mimi tuna mchanganyiko mzuri kati ya vijana na wakongwe, na mwishowe vijana wanaendelea kujifunza kila siku na wachezaji wengine wenye uzoefu zaidi wanajaribu kutufunsidha.”

“Nadhani mchanganyiko huu una faida nyingi katika nyanja nyingi, kwa sababu kundi hili ni la kuvutia, na lazima tuwe wenyewe kwasababu tunajua kile tunachoweza kufanya tukiwa sisi wenyewe.”

Hakuishia hapo aliongeza kusema kuwa hatwana Lionel Messi au Neymar, lakini wana wachezaji ambao kila mmoja ana mchango mkubwa zaidi, kama Pedri, Gavi, Busquets, Asensio kwa kiwango alicho nacho na watatusaidia.garciaQatar itakuwa ladha ya kwanza kwa Garcia kucheza Kombe la Dunia akiwa na Uhispania, na anafurahi kuwa sehemu ya timu, akielezea jinsi alivyotazama mashindano ya zamani tangu utoto. Alisema kuwa unapozeeka, unafikiria unatamani ungekuwa huko siku moja na ni fursa ya kuwa hapa kuishi uzoefu ambao kila mtu angependa kuishi hivyo ni lazima kuthaminiwa.

Garcia anatarajia kuchaguliwa katika kikosi cha Luis Enrique kwa ajili ya mchezo wa ufunguzi wa Uhispania dhidi ya Costa Rica siku ya Jumatano, na kuongeza kuwa ushindani katika kila nafasi ni mkubwa sana, lakini kichwani kwake ni kufanya kazi kadri awezavyo katika mazoezi ili awe katika kiwango cha juu zaidi kila dakika.

Baada ya kukutana na Costa Rica, Uhispania itamenyana na Ujerumani na Japan katika Kundi E.

Acha ujumbe