Japan, moja ya timu safi zaidi ya Kombe la Dunia, ilifanya fujo kidogo wakati wa mikwaju ya penalti na inaweza kuchukua muda kusafisha maumivu ya moyo kutokana na matokeo waliyoyapata.

Wamepata marafiki wengi kwa kusafisha vyumba vya kubadilishia nguo baada ya michezo na kuwa moja ya timu za mfano, lakini safari yao imeishia hatua ya 16 bora baada ya kutolewa kwa mikwaju ya penati 1-3 dhidi ya Croatia.
Japan walikutana na moja ya timu bora sana Croatia, iliyoshinda mara mbili kwa mikwaju ya penati kwenye njia yao ya kutinga fainali nchini Urusi, miaka minne iliyopita, na hapa walikuwa na kipa mzuri zaidi Dominik Livakovic aliyeibuka shujaa.

Livakovic aliokoa penalti tatu na Mario Pasalic akafunga penalti na kuipeleka timu ya Zlatko Dalic kutinga hatua ya nane bora. Kupitia Meridianbet unaweza kubeti kama Croatia atavuka kuingia nusu fainali, kwenye machaguo spesho.
Japan wanatoka nje katika hatua hii kwa mara ya nne. Hawajawahi kuwa zaidi. Lakini hawakuweza kurudia matokeo makubwa dhidi ya Ujerumani na Hispania katika hatua ya makundi.

Walichukua bao la kuongoza kipindi cha kwanza dakika mbili kabla ya muda wa mapumziko, baada ya kuamsha shinikizo mwishoni mwa kipindi cha kwanza. Kabla ya Perisic kusawazisha na mpaka dakika 90 zinakamilika ubao ulikuwa ni 1-1.
Kanuni ikatumika zikaongezwa dakika 30, ili kukamilisha zile dakika 120, lakini napo milango ya pande zote mbili ilikuwa ni migumu hali iliyopelekea maamuzi yafanyike kwa njia ya tatu ya mikwaju ya penati.


