Eng. Hersi Said Aandika Historia Mpya Katika Soka la Dunia

Rais wa Klabu ya Yanga SC na Mwenyekiti wa Chama cha Vilabu Afrika (ACA), Eng. Hersi Said, ameandika historia mpya baada ya kuteuliwa rasmi na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) kuwa Mjumbe wa Kamati ya Mashindano ya Vilabu ya Wanaume Duniani kwa kipindi cha miaka minne (2025–2029).

Eng. Hersi Said Aandika Historia Mpya Katika Soka la Dunia

Kwa uteuzi huu, Eng. Hersi anakuwa mtu wa kwanza kutoka Afrika Mashariki na Kati kuingia katika moja ya kamati kubwa na zenye ushawishi mkubwa ndani ya FIFA, hatua inayodhihirisha kuaminika kwake kimataifa na mchango wake katika maendeleo ya soka barani Afrika.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa.

Eng. Hersi Said Aandika Historia Mpya Katika Soka la Dunia

Kwa mujibu wa barua rasmi ya FIFA iliyotiwa saini na Naibu Katibu Mkuu, Mattias Grafström, uteuzi huo unazingatia kanuni za FIFA na taratibu za utawala bora. Eng. Hersi Said anatarajiwa kupokea maelekezo ya awali kupitia barua pepe ili kurasimisha taarifa zake binafsi kwa ajili ya kuanza rasmi majukumu yake.

Uteuzi huu ni ishara ya kuongezeka kwa ushawishi wa viongozi wa soka wa Afrika Mashariki katika meza za maamuzi ya kimataifa, na unatarajiwa kufungua milango zaidi kwa maendeleo ya vilabu vya kanda hii.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.