Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetangaza rasmi kufunguliwa kwa Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi uliopo Tabora, baada ya kukamilika kwa marekebisho yaliyokidhi vigezo vya kikanuni na sheria za mpira wa miguu.
Ali Hassan Mwinyi ulifungiwa kutokana na changamoto za miundombinu, ambazo zilikuwa haziruhusu kutumika kwa michezo ya Ligi kama ilivyoainishwa kwenye Kanuni ya Leseni za Klabu. Baada ya ukaguzi wa kina, TFF imejiridhisha kuwa marekebisho yaliyofanyika yamekidhi masharti yote ya kikanuni.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa.
TFF imezitaka klabu zote kuendelea kuboresha na kutunza miundombinu ya viwanja vyao vya nyumbani, kwa kushirikiana na wamiliki wa viwanja (hasa kwa klabu zisizomiliki viwanja), ili kuhakikisha michezo ya Ligi inachezwa katika mazingira bora yanayoongeza ushindani, usalama na thamani ya Ligi.
Hatua hii ni ishara ya dhamira ya TFF kuimarisha mazingira ya soka nchini, hasa katika mikoa ya pembezoni, na kuleta fursa zaidi kwa mashabiki kushuhudia mechi za kiwango cha juu katika viwanja vyao vya nyumbani.