Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limemteua rasmi Oscar Mirambo kuwa Kaimu Katibu Mkuu wa shirikisho hilo kuanzia Oktoba 1, 2025.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisa Habari na Mawasiliano wa TFF, Cliford Mario Ndimbo, uteuzi huo unakuja kufuatia kumalizika kwa mkataba wa aliyekuwa Katibu Mkuu, Kidao Wilfred, ambao unahitimishwa tarehe 30 Septemba 2025.


