Mwanariadha mahiri wa Tanzania, Alphonce Felix Simbu, ameandika historia mara mbili ndani ya wiki moja, kwanza kwa kutwaa medali ya dhahabu katika Mashindano ya Dunia ya Riadha jijini Tokyo, Japan, na pili kwa kupandishwa cheo jeshini kutoka Sajini hadi Sajini Taji (Staff Sergeant) ndani ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Cheo hicho kipya kilitolewa rasmi na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Jacob John Mkunda, katika hafla maalum iliyofanyika Septemba 25, 2025, makao makuu ya jeshi Upanga, Dar es Salaam. Jenerali Mkunda alisifu nidhamu, uzalendo, na bidii ya Simbu, akisema ushindi wake si wa mtu binafsi tu bali ni fahari kwa taifa zima na bara la Afrika.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa.


