Napoli Wameweka Tarehe ya Mwisho kwa Galatasaray Kukamilisha Dili la Osimhen.

Napoli wameipa Galatasaray tarehe ya mwisho ya kuwasilisha nyaraka zote muhimu za usajili wa Victor Osimhen, baada ya pande zote mbili kukubaliana kuhusu kipengele kinachozuia uhamisho kwenda klabu nyingine za Serie A na masuala ya mgao wa asilimia ya mauzo ya baadaye.

Napoli Wameweka Tarehe ya Mwisho kwa Galatasaray Kukamilisha Dili la Osimhen.

Majadiliano haya yamechukua muda mrefu majira haya ya kiangazi, baada ya mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Nigeria kutumia msimu uliopita kwa mkopo Galatasaray, ambako alifunga mabao 37 katika mechi 41 rasmi na kutoa pasi za mabao 8.

Pia meridianbet inatoa michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile, Aviator, poker, Roullette, sloti na mingine kibao. Ingia meridianbet na ucheze sasa.

Ingawa mkataba upo karibu kukamilika, Napoli hawako tayari kusubiri milele. Subira yao imepungua, na sasa wameweka tarehe ya mwisho kuwa Jumatatu, wakiamini kuwa Galatasaray ina muda wa kutosha kukamilisha nyaraka zote zinazohitajika.

Masuala magumu tayari yameafikiwa €40 milioni italipwa papo hapo, €35 milioni zitalipwa kwa awamu hadi kufikia Juni 2026.

Napoli Wameweka Tarehe ya Mwisho kwa Galatasaray Kukamilisha Dili la Osimhen.

Kitu muhimu zaidi ni kwamba Galatasaray wamekubali kuweka kipengele cha faini kubwa iwapo Osimhen atauzwa kwa klabu nyingine ya Serie A ndani ya miaka miwili ijayo.

Hitilafu ya mwisho ilikuwa ni kuhusu asilimia ya mauzo ya baadaye, lakini Napoli hawataweka mkazo sana kwenye hilo, wakikubali kuwa si sehemu ya msingi ya dili hili.

Kwa maslahi ya pande zote, hasa Osimhen mwenyewe, dili hili linapaswa kukamilika haraka iwezekanavyo.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.