Chelsea Kupapatuana na Liver, Arsenal, United Kumpata Ayyoub Bouaddi

Kwa mujibu wa ripoti, Chelsea ni miongoni mwa vilabu vya Ligi Kuu England vinavyomvizia kiungo wa Lille, Ayyoub Bouaddi.

Chelsea Kupapatuana na Liver, Arsenal, United Kumpata Ayyoub Bouaddi

The Blues walikuwa aktivi sana katika dirisha la majira ya kiangazi, wakifanya uwekezaji mkubwa kwenye kikosi chao, hasa katika safu ya ushambuliaji ambako walisajili wachezaji watano wapya.

Huku dirisha la usajili la Januari likikaribia, haitegemewi The Blues kuwa na shughuli nyingi, ingawa katika soka mambo hubadilika haraka.

Mashabiki wangependa kuona angalau usajili mmoja au miwili ya kikosi cha kwanza mwezi Januari, lakini hilo linaonekana kuwa gumu kutokea. Hata hivyo, The Blues inaendelea kuwafuatilia kwa karibu wachezaji wa baadaye.

Tayari The Blues wamekubaliana kusajili mchezaji wa miaka 16, Deinner Ordonez, huku Mohamed Zongo akitarajiwa kujiunga na Strasbourg kwa mpango wa baadaye kuichezea The Blues. Bouaddi ameonyesha kiwango kizuri akiwa Lille msimu huu.

Chelsea Kupapatuana na Liver, Arsenal, United Kumpata Ayyoub Bouaddi

Hata hivyo, inaonekana kuna jina jingine jipya kwenye rada ya Chelsea, ambapo Caught Offside wameripoti kuwa The Blues ni miongoni mwa vilabu vinavyomtaka Bouaddi.

Ripoti hiyo inaongeza kuwa Manchester United na Arsenal pia wanamfuatilia kwa karibu kiungo huyo wa miaka 18. Chelsea wanaweza kutoa dau la kati ya euro milioni 45 hadi 50 mwezi Januari na kisha kumtoa kwa mkopo Strasbourg, ingawa Lille wanadaiwa kushikilia bei ya euro milioni 60.

Bouaddi, ambaye tayari aliwahi kuhusishwa na Chelsea hapo awali, ameshacheza mechi 20 katika mashindano yote msimu huu na ni mhimili muhimu wa kikosi cha Lille ambacho kwa sasa kinashika nafasi ya nne kwenye Ligue 1.

Bado haijulikani kama Chelsea wataamua kusajili kiungo mwezi Januari, lakini kuna uwezekano mkubwa wakaongeza mchezaji wa nafasi hiyo msimu ujao.

Chelsea Kupapatuana na Liver, Arsenal, United Kumpata Ayyoub Bouaddi

Ripoti zinaeleza kuwa Chelsea wanapanga kumsajili kiungo mpya msimu ujao ili kupunguza mzigo kwa Moises Caicedo na Enzo Fernandez.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.