IBENGE ANATAKA KUWA KOCHA WA KUKUMBUKWA AZAM FC

Hesabu za Kocha Mkuu wa Azam FC raia wa DR Congo, Florent Ibenge ni kutengeneza hadithi tamu na ya kukumbukwa daima ndani ya timu hiyo kutoka mitaa ya Chamanzi.

IBENGE ANATAKA KUWA KOCHA WA KUKUMBUKWA AZAM FC

Ibenge amebakiza dakika 90 tu kuandika historia hiyo ambayo haijawahi kutokea ndani ya timu hiyo tangu kuanzishwa kwake, takribani miaka 20 sasa.

Azam FC, imeanza vyema tiketi ya kuisaka hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika baada ya juzi kuibuka na ushindi wa mabao 2-0, dhidi ya Kikosi Maalumu cha Kuzuia Magendo, KMKM kutoka Zanzibar.

Katika mechi hiyo ya kwanza iliyopigwa Kwenye Uwanja wa New Amaan Complex visiwani Zanzibar, mabao ya Azam yalifungwa na mshambuliaji, Jephte Kitambala Bola dakika ya 6, huku lingine likifungwa na beki wa kushoto wa kikosi hicho, Pascal Msindo kunako dakika ya 42.

Timu hizo zitarudiana Oktoba 24, 2025 kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar, kama wakishinda au kupata matokeo chanya watakuwa wamefuzu hatua ya makundi kwa mara ya kwanza kwenye historia yao.

IBENGE ANATAKA KUWA KOCHA WA KUKUMBUKWA AZAM FC

Rekodi kubwa ya Azam katika Michuano ya CAF ni kutolewa raundi ya pili ya Kombe la Shirikisho Afrika mwaka 2013 na FAR Rabat ya Morocco kwa mabao 2-1, iliyofungwa ugenini baada ya kulazimishwa suluhu 0-0, kwenye mchezo wa kwanza nyumbani.

Katika raundi ya awali mwaka huo wa 2013, Azam ilipata ushindi wa mabao 8-1 dhidi ya El Nasir ya Sudan Kusini kisha kuitupa nje Barrack Young Controller II ya Liberia kwa mabao 2-1 na mara zote ilizoshiriki Kombe hilo na Ligi ya Mabingwa Barani Afrika imekuwa ikiishia njiani, Ingawa safari hii kuna uwezekano mkubwa ikaandika rekodi mpya chini ya Mkongomani Florent Ibenge.

Ibenge aliyetambulishwa na kikosi hicho, Julai 5, 2025, akitokea Al Hilal Omdurman ya Sudan, akirithi nafasi ya Kocha, Mmorocco Rachid Taoussi, ndiye aliyebeba matumaini makubwa ya kikosi hicho ya kusaka rekodi mpya ambayo haijawahi kuandikwa na timu hiyo tangu ilipoasisiwa mwaka 2004.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.