ISHU YA KOCHA MPYA YANGA, MABOSI WAPATA KIGUGUMIZI

Ukipiga simu kwenye uongozi wa klabu ya Yanga kuuliza nini mustakabali wao juu ya nani atakuwa kocha mkuu ajaye baada ya Roman Folz kuondoka, utachoambulia ni kuwa mchakato unaendelea na huku mtaani taarifa zikiwa Romuald Rakotondrabe ‘Roro’ ndiye amekuwa tageti kuu.

ISHU YA KOCHA MPYA YANGA, MABOSI WAPATA KIGUGUMIZI

Ukweli ni kwamba Yanga wameanza upya mchakato wa kutafuta kocha wa timu hiyo baada ya mmoja wa viongozi kuweka wazi kuwa uwezekano wa kumchukua kocha Roro aliyekuwa anakaribia kutua katika timu hiyo, bila kutaja sababu za dili hilo kusuasua.

Uamuzi huo unakuja baada ya Yanga kuachana na aliyekuwa kocha wao Romain Folz, baada ya timu hiyo kupoteza mechi ya kwanza msimu huu ikifungwa bao 1-0 ugenini dhidi ya Silver Strikers ya Malawi yenye kiungo bora Uchizi Vunga.

Mechi hiyo ya mkondo wa kwanza hatua ya pili ya Ligi ya Mabingwa Afrika, imeiweka Yanga kwenye nafasi ya kutakiwa lazima ishinde angalau kwa tofauti ya mabao 2-0 katika mechi ya marudiano itakayopigwa Oktoba 25, 2025 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar.

Folz ambaye ameiongoza Yanga kwenye mechi sita za mashindano, ameshinda nne na sare moja, timu yake ikifunga mabao tisa huku bao pekee ililoruhusu Malawi ndio lililohitimisha maisha yake ndani ya klabu hiyo, akichukua taji moja la Ngao ya Jamii.

ISHU YA KOCHA MPYA YANGA, MABOSI WAPATA KIGUGUMIZI

Timu hiyo sasa itakuwa chini ya kocha Patrick Mabedi aliyekuwa msaidizi wa Folz wakati Yanga ikitafuta kocha mpya wa kuendelea na majukumu ya kukinoa kikosi hicho.

Taarifa kutoka ndani ya uongozi wa juu wa Yanga ni kwamba, klabu hiyo haitaendelea na hesabu za kumchukua Roro ambapo mchakato huo umegeuziwa kwa kocha mpya mwingine.

Bosi mmoja wa juu amesema kuwa mchakato wa Roro hautaendelea kufuatia uongozi wao kuachana naye kwa sababu ambazo hata hivyo hawakutaka kuziweka wazi.

“Ni kweli tulikuwa na hesabu za kumchukua kocha Rakotondrabe (Roro) lakini kuna mambo yametupa wasiwasi, hatutaweza kuendelea na huo mpango tena.

“Tutarudi kuanza mchakato upya kabisa, tunataka kufanya mambo kwa umakini zaidi, tupate kocha ambaye atatupa kile ambacho tunakitarajia kama klabu,” alisema bosi huyo kutoka kwenye kamati tendaji ya timu hiyo.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.