Yildiz Amshukuru Tudor Baada ya Kutimuliwa Juventus

Mchezaji wa Juventus, Kenan Yildiz, ametuma salamu za heri kwa Igor Tudor, aliyefutwa kazi kama kocha mkuu wa Juventus siku ya Jumatatu, akisema: “Kila la heri kwa siku zijazo.”

Yildiz Amshukuru Tudor Baada ya Kutimuliwa Juventus

Juventus walithibitisha rasmi kuachana na Tudor kama kocha mkuu baada ya mfululizo wa michezo minane bila ushindi katika Serie A na Ligi ya Mabingwa. Kikosi hicho cha Bianconeri hakikushinda tangu walipoibuka na ushindi wa mabao 4-3 dhidi ya Inter mnamo Septemba 13, na hakikuweza kufunga katika mechi nne za mwisho chini ya uongozi wa Tudor.

Kocha huyo raia wa Kroatia ndiye meneja wa kwanza kufutwa kazi katika Serie A msimu wa 2025-26, akiondolewa baada ya michezo minane pekee ya ligi.

Gleison Bremer alikuwa wa kwanza kati ya wachezaji wa Juventus kutoa shukrani kwa Tudor baada ya habari za kufutwa kwake kusambaa Jumatatu. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Yildiz aliandika,“Asante kwa kila kitu, kocha. Nakutakia mafanikio katika siku zijazo.”

Yildiz Amshukuru Tudor Baada ya Kutimuliwa Juventus

Ikumbukwe kuwa Juventus kwenye mechi 5 za mwisho kwenye mashindano yote hawajashinda mechi hata moja, wametoa sare mbili na kupoteza mechi 3 mfululizo.

Kesho watakuwa Allianz pale kusaka ushindi dhidi ya Udinese Calcio. Je wanaweza kuondoka na ushindi?. Bashiri na Meridianbet mechi zote hapa.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.