Manchester City Waishangaza Anfield, Bernardo na Haaland Wabadilisha Mchezo

Pale ambapo wengi walidhani Manchester City wameondoka kabisa katika kinyang’anyiro cha ubingwa Ligi Kuu ya Uingereza, Bernardo Silva na Erling Haaland wamejitokeza wakiwaacha Liverpool wakiwa na mshangao na Arsenal wakitazama kwa hofu.

Manchester City Waishangaza Anfield, Bernardo na Haaland Wabadilisha Mchezo

Anfield imekuwa ngome isiyopinduliwa kwa Liverpool, lakini mechi ya Jana ilionyesha kitu kisichowahi kushuhudiwa, matokeo ambayo hayajaonekana tangu mwaka 2003.

Ushindi wa mwisho wa City Anfield mbele ya mashabiki ulikuwa mwaka 2003, wakati Kevin Keegan akiwa meneja, Maine Road ikiwa uwanja wao, na Peter Schmeichel akiwa mlinda mlango. Pep Guardiola amekuwa akikosa kabisa matokeo Anfield, lakini hapo jana, kocha huyo Muhispania aliandika kumbukumbu mpya kama kocha wa Manchester City.

Nusu ya kwanza ilionekana kuwa ni ya City, wakidhibiti mpira na kushambulia kwa ufanisi. Lakini Liverpool walijitokeza, na Dominik Szoboszlai aliweka kimyani kwa shuti la faulu na kuipa Liverpool bao la kuongoza, wakiwacha City nyuma.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Manchester City Waishangaza Anfield, Bernardo na Haaland Wabadilisha Mchezo

Hata hivyo, Bernardo Silva, kiungo wa Kireno hakukubali kuanguka, na aliwarudisha Manchester City mchezoni na bao la kusawazisha dakika ya 82. Baada ya hapo, Haaland aliongeza bao la pili na la ushindi kwa penalti, huku Gianluigi Donnarumma akifanya kazi ya ziada na kuzuia mashambulizi ya hatari kutoka kwa Liverpool waliokuwa wakitafuta bao la kusawazisha.

Katika dakika za mwisho kabisa za mchezo, kilishuhudiwa kitu cha ajabu baada ya bao la Rayan Cherki kutoka kwenye mstari wa nusu uwanja kukataliwa huku Szoboszlai akitolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya kumvuta jezi Erling Haaland.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.