Azam FC Yaelekea Casablanca Kuivaa Wydad AC

Kikosi cha Azam FC kimeondoka nchini alfajiri ya leo, Jumatano, kuelekea Casablanca, Morocco kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wao muhimu wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Wydad AC. Huu ni mchezo ambao Azam FC wanaitaji matokeo ya ushindi pekee ili kupata nafasi ya kufuzu kuingia hatua ya robo fainali.

Azam FC Yaelekea Casablanca Kuivaa Wydad AC

Msafara huo umejumuisha wachezaji kadhaa muhimu katika kila idara, huku makipa Aishi Manula, Zuberi Foba na Antony Mpemba wakiongoza safu ya walinda mlango.

Azam FC Yaelekea Casablanca Kuivaa Wydad AC

Katika safu ya mabeki, Azam FC imewasafirisha Lusajo Mwaikenda, Pascal Msindo, Lameck Lawi, Twalib Nuru, Yoro Diaby, Nathaniel Chilambo, Ben Zitoune na Yeison Fuentes, wakitarajiwa kuwa nguzo imara katika kuzuia mashambulizi ya wenyeji wao.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Azam FC Yaelekea Casablanca Kuivaa Wydad AC

Kiungo cha timu hiyo kitaundwa na nyota kama Himid Mao, Feisal Salum, James Akaminko, Yahya Zayd, pamoja na wengine akiwemo Cheickna Diakite na Pape Doudou, ambao wanatarajiwa kuongoza mapambano katikati ya uwanja.

Upande wa ushambuliaji utategemea nguvu ya Jephte Kitambala, Zidane Sereri na JJ Ngita kusaka mabao muhimu ugenini.

Azam FC Yaelekea Casablanca Kuivaa Wydad AC

Azam FC inaelekea Morocco ikiwa na matumaini makubwa ya kupata matokeo chanya dhidi ya Wydad AC, katika mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa. Mashabiki wa soka nchini watakuwa wakifuatilia kwa karibu kuona kama wawakilishi hao wa Tanzania watafanikiwa kushinda na kufuzu hatua ya robo fainali.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.