Klabu ya Real Madrid imeanza mchakato wa kusaka kocha mpya baada ya kutolewa katika michuano ya UEFA Champions League kufuatia kipigo cha mabao 4-3 (jumla 6-4) dhidi ya Bayern Munich katika mchezo uliopigwa mjini Munich.
Uongozi wa klabu hiyo chini ya rais Florentino Pérez umeanza kuangalia machaguo mbalimbali ya makocha watakaochukua nafasi hiyo msimu ujao, huku lengo likiwa ni kurejesha ubora wa timu katika mashindano ya Ulaya.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Miongoni mwa majina yanayoripotiwa kuingia kwenye orodha hiyo ni Jürgen Klopp, ambaye anatajwa kuwa kipaumbele cha juu, ingawa bado hakuna mawasiliano rasmi yaliyofanyika kati yake na klabu hiyo ya Hispania.
Pia kocha Mauricio Pochettino anatajwa kuwa mgombea mwenye nafasi kubwa zaidi kutokana na urahisi wa kupatikana kwake, huku Zinedine Zidane na Didier Deschamps nao wakiwekwa kwenye orodha ya mbadala wanaofikiriwa.
Kushindwa kwa kocha Álvaro Arbeloa kuifikisha timu hiyo hatua ya juu zaidi katika mashindano ya Ulaya kumechochea uongozi wa Real Madrid kuanza upya mipango ya benchi la ufundi, huku mustakabali wake ukiwa bado haujathibitishwa.

