Samatta Afunga Bao la Kwanza Le Havre, Aweka Rekodi Ulaya

Nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta, hatimaye amefungua akaunti ya mabao akiwa na Le Havre AC baada ya kufunga katika sare ya 1-1 dhidi ya wapinzani wao kwenye mchezo wa Ligue 1 uliochezwa Jumapili, Aprili 12, 2026.

Samatta Afunga Bao la Kwanza Le Havre, Aweka Rekodi UlayaMchezo huo ulipigwa katika Uwanja wa Allianz Riviera, ambapo Samatta aliipatia timu yake bao la kuongoza dakika ya 41 kwa kumalizia pasi safi kutoka kwa Rassoul Ndiaye.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Bao hilo linakuwa la kwanza kwa mshambuliaji huyo tangu ajiunge na Le Havre katika dirisha kubwa la usajili la majira ya kiangazi, baada ya kukaa muda bila kufunga tangu aanze kuitumikia klabu hiyo ya Ufaransa.

Samatta Afunga Bao la Kwanza Le Havre, Aweka Rekodi UlayaKatika mchezo huo, Samatta alionyesha kiwango kizuri kabla ya kutolewa nje dakika ya 87 na nafasi yake kuchukuliwa na Stephan Zagadou, huku timu hizo zikigawana pointi mojamoja.

Mafanikio hayo yanaendelea kuonyesha mchango wa Samatta katika soka la kimataifa, hasa akiwa nahodha wa Taifa Stars na mchezaji tegemeo katika kikosi chake cha sasa.

Samatta Afunga Bao la Kwanza Le Havre, Aweka Rekodi UlayaKwa bao hilo, Samatta ameweka rekodi ya kipekee kwa kufunga katika ligi tano tofauti barani Ulaya, hatua inayodhihirisha uzoefu na ubora wake katika soka la ushindani wa juu.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.