Kocha wa Luis Enrique wa Paris Saint-Germain ametoa majibu baada ya timu yake kushinda 2-0 katika uwanja wa Anfield na kusonga mbele kwa ushindi wa jumla wa 4-0 dhidi ya Liverpool kwenye robo fainali ya Ligi ya Mabingwa.

Luis Enrique amekiri kwamba timu yake ya Paris Saint-Germain ilikuwa na bahati kutofungwa na Liverpool, huku ikifanikiwa kufuzu nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa.
Ousmane Dembele alifunga mabao mawili ya dakika za mwisho na kuipa timu ya mabingwa ushindi wa 2-0 katika uwanja wa Anfield uliokuwa na mvua Jumanne usiku kwenye mchezo wa marudiano wa robo fainali, na kukamilisha ushindi wa jumla wa mabao 4-0.
Baada ya kipindi cha kwanza kilichokuwa kigumu na cha ushindani mkali, Liverpool walitawala mchezo kwa muda mrefu lakini walishindwa kutumia vyema nafasi walizopata kabla ya bao la kwanza la Ousmane Dembele dakika ya 72 kumaliza kabisa matumaini ya ushindani katika mchezo huo.
Luis Enrique alisema: “Ilkuwa mechi muhimu kwetu, mechi ya kiwango cha juu si tu kwa mashabiki wetu au wa Liverpool bali kwa mashabiki wote. Timu mbili nzuri sana, Liverpool walicheza mchezo wa kuvutia, wenye kasi na nguvu nyingi. Ilikuwa mechi ya ushindani mkali sana.”

Kulikuwa na nyakati chache ambapo sisi tulikuwa na faida. Mambo yalizidi kuwa magumu zaidi kwetu kipindi cha pili lakini tulionyesha aina ya timu tuliyo. Ilikuwa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa ya kuvutia sana. Alisema kocha huyo.
Luis Enrique alisema: “Liverpool walistahili kabisa kufunga bao katika kipindi chote cha mchezo.”
Kocha huyo alisema kuwa kama wangelifungwa bao mapema, ingekuwa ngumu sana kwao hivyo unahitaji mambo yaende upande wako. Ni jambo la kufurahisha kuwa na wachezaji wa aina hii klabuni, na pia mashabiki msaada wao ulikuwa wa kipekee. Wanafurahi kuwaonyesha wao ni timu yaaina gani.
Enrique aliongeza: “Liverpool walilazimika kuchukua hatari kubwa, na hilo lilitupa nafasi ya kufanya mashambulizi ya kushtukiza na kuumaliza mchezo. Ilichukua muda mrefu zaidi kuliko nilivyotarajia kufanya hivyo.”
“Lakini tulijilinda vizuri, Matvey Safonov alikuwa muhimu sana, na tulidhibiti mambo tuliyoweza kuyadhibiti. Tulijua wanapaswa kuchukua hatari. Mara tu tulipofunga bao la kwanza, mambo yalibadilika. Kabla ya mchezo tulijua tunaweza kupata wakati mgumu na kuteseka nyakati fulani, lakini nadhani tuliudhibiti mchezo vizuri sana.”
Baada ya ushindi huo PSG sasa wanamsubiri kati ya Bayern Munich au Real Madrid kwenye hatua ya Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

