Ousmane Dembélé Apongeza Ushindi wa Paris Saint-Germain Dhidi ya Liverpool FC

Mshambuliaji wa Paris Saint-Germain, Ousmane Dembélé, ameipongeza timu yake kwa uvumilivu mkubwa waliouonyesha katika ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Liverpool FC kwenye mchezo wa marudiano wa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya uliochezwa Anfield.

Ousmane Dembélé Apongeza Ushindi wa Paris Saint-Germain Dhidi ya Liverpool FCDembélé alisema kuwa mchezo huo ulikuwa mgumu kutokana na presha kubwa ya wapinzani, licha ya PSG kuwa na faida ya mabao 2-0 kutoka mchezo wa kwanza.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

“Ni robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, uwanjani kama hapa, na ingawa tulikuwa tumeshinda 2-0 mchezo wa kwanza tulijua itakuwa ngumu,” alisema Dembélé

Ousmane Dembélé Apongeza Ushindi wa Paris Saint-Germain Dhidi ya Liverpool FCAliongeza kuwa katika michuano ya kiwango cha juu kama hiyo, hakuna mechi rahisi na kila timu inalazimika kupambana hadi mwisho.

“Hakuna mechi rahisi kwenye Ligi ya Mabingwa. Unapaswa kuteseka kama unataka kufika mbali kwenye mashindano haya,” alisisitiza.

Paris Saint-Germain ililazimika kuvumilia mashambulizi makali kutoka kwa Liverpool FC, ambao walipata mashuti 21 langoni katika kipindi cha pili, hasa katika mazingira magumu ya mvua na upepo mkali.

Ousmane Dembélé Apongeza Ushindi wa Paris Saint-Germain Dhidi ya Liverpool FCDembélé alifunga bao la kwanza dakika ya 72 kabla ya kuongeza la pili katika dakika za majeruhi, akihakikisha PSG inatinga hatua ya nusu fainali kwa ushindi wa jumla wa 4-0.

“Tulikuwa na nafasi kipindi cha kwanza. Nilihisi tulidhibiti mchezo kipindi cha kwanza, lakini kipindi cha pili kilikuwa kigumu zaidi, jambo la kawaida kwenye Ligi ya Mabingwa,” alisema.

Katika hatua inayofuata, PSG itakutana na mshindi kati ya Real Madrid au Bayern Munich katika nusu fainali, huku mechi ya kwanza ikitarajiwa kuchezwa Paris Aprili 28 au 29.

Ousmane Dembélé Apongeza Ushindi wa Paris Saint-Germain Dhidi ya Liverpool FCDembélé, ambaye alikosa sehemu kubwa ya msimu kutokana na majeraha, amesema anaendelea kujituma kuhakikisha anaisaidia PSG kwa njia zote iwe kufunga, kutoa pasi za mabao au kushambulia kwa bidii, akiahidi kumaliza msimu akiwa katika kiwango bora zaidi.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.