Singida Black Stars Kwenda Sauzi Kusaka Heshima

Kocha Mkuu wa Singida Black Stars, David Ouma, amesema kikosi chake kinaelekea Afrika Kusini kikiwa na lengo la kulinda heshima katika mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Stellenbosch FC. Mchezo huo utapigwa Jumapili kuanzia saa 1:00 usiku, huku timu zote zikiwa tayari zimepoteza nafasi ya kufuzu hatua inayofuata.

Ouma amesema ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Fountain Gate kwenye ligi ya ndani umeongeza morali ya wachezaji, na kwa sasa hakuna majeruhi kikosini. Ameeleza kuwa licha ya kutokuwa na nafasi ya kusonga mbele, timu hiyo itaingia uwanjani kwa nidhamu, ushindani na heshima kwa mashindano hayo ya kimataifa.

Singida Black Stars Kwenda Sauzi Kusaka Heshima

“Hatuna cha kupoteza. Kufika hapa tayari ni hatua kubwa kwetu kwa sababu ni mara yetu ya kwanza kushiriki mashindano haya. Tumejifunza mengi, ikiwemo namna ya kuutumia vizuri uwanja wa nyumbani,” amesema Ouma, akisisitiza kuwa uzoefu walioupata utakuwa msingi wa mafanikio yajayo.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Singida Black Stars Kwenda Sauzi Kusaka Heshima

Katika Kundi C, vinara ni CR Belouizdad inayofundishwa na Sead Ramovic, ikiwa na pointi 12, huku AS Otoho d’Oyo wakishika nafasi ya pili kwa pointi tisa. Timu zote mbili tayari zimefuzu hatua inayofuata. Singida ipo nafasi ya tatu ikiwa na pointi nne, sawa na Stellenbosch walioko mkiani.

Singida Black Stars Kwenda Sauzi Kusaka Heshima

Mchezo wa kwanza kati ya Singida na Stellenbosch uliopigwa Novemba 30, 2025 katika Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar, ulimalizika kwa sare ya bao 1-1. Stellenbosch walitangulia kupitia Langelihle Phili dakika ya 52 kabla ya Singida kusawazisha dakika ya 90+1 kupitia Marouf Tchakei. Mechi ya Jumapili itakuwa ya kusaka heshima, huku kila upande ukilenga kumaliza hatua ya makundi kwa matokeo chanya.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.