Romero amekuwa akihusishwa na kuondoka Spurs kufuatia kauli yake ya hivi karibuni kupitia akaunti yake rasmi ya Instagram.
Mchezaji huyo wa Argentina aliwakosoa maamuzi ya viongozi wa Spurs mara baada ya dirisha la usajili kufungwa, akitaja hali ya kukosekana kwa wachezaji wa kikosi cha kwanza kutokana na majeraha kuwa ni “ya aibu”.
Nahodha huyo wa Tottenham alihusishwa na kuondoka kaskazini mwa London majira ya joto yaliyopita, huku Atletico Madrid wakimfuatilia beki huyo, ambaye hatimaye alisaini mkataba mpya na mabingwa wa Europa League.
Hata hivyo, inaripotiwa kuwa Romero amekata tamaa na maisha katika Uwanja wa Tottenham Hotspur huku Spurs wakihangaika katika nafasi za chini za msimamo wa ligi.
Tottenham Spurs walipoteza 2-1 dhidi ya Newcastle Jumanne usiku, matokeo yaliyofanya wawe na ushindi mbili tu katika mechi 17 zilizopita za ligi na kuwaacha pointi tano tu juu ya eneo la kushuka daraja.
Kipigo hicho cha nyumbani katikati ya wiki kilimgharimu Thomas Frank kazi yake kama kocha wa Spurs, huku klabu hiyo ikianza kutafuta kocha mpya kabla ya Derby ya London Kaskazini ya wiki ijayo.