Klabu ya Tottenham Hotspur imetangaza rasmi kufanya mabadiliko katika benchi la ufundi la timu ya wanaume, ambapo Kocha Mkuu Thomas Frank ameondoka leo.
Kupitia taarifa iliyotolewa na klabu hiyo, imeeleza kuwa Thomas, ambaye aliteuliwa mwezi Juni 2025, alipewa muda na sapoti ya kutosha ili kuijenga timu na kuweka msingi imara wa mafanikio ya baadaye.
Hata hivyo, mwenendo wa matokeo na kiwango cha uchezaji wa timu hiyo umeifanya Bodi ya Wakurugenzi kufikia uamuzi wa kufanya mabadiliko katika hatua hii ya msimu.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Tottenham imeeleza kuwa katika kipindi chote alichohudumu klabuni hapo, Thomas Frank alionesha kujituma kwa kiwango cha juu na kufanya kila juhudi kuhakikisha timu inapiga hatua.
Klabu hiyo imemshukuru kwa mchango wake na kumtakia kila la heri katika safari yake ijayo ya ukocha.