Newcastle Wanapanga Mazungumzo na Howe huku Wakiangalia Uwezekano wa Kumuuza Gordon.

Newcastle United watafanya mazungumzo ya mwisho wa msimu huku Eddie Howe akikutana na Yasir Al-Rumayyan pamoja na viongozi wa Public Investment Fund kujadili matokeo ya timu na mipango ya maendeleo, wakati nafasi ya kushiriki michuano ya Ulaya bado ipo katika mechi tano zilizosalia za ligi.

Newcastle Wanapanga Mazungumzo na Howe huku Wakiangalia Uwezekano wa Kumuuza Gordon.

Inaripotiwa pia kuwa klabu hiyo itazingatia kumuuza Anthony Gordon kwenda nje ya nchi pekee, huku Bayern Munich wakitajwa kuwa miongoni mwa wanaomvizia, ili kuepuka kuziimarisha timu pinzani za ndani kama Arsenal au Liverpool. Wakati huo huo, Newcastle wameanza mazungumzo ya kumsajili winga wa thamani ya pauni milioni 43, Eduardo Conceicao.

Howe anatarajiwa kukutana na Al-Rumayyan na viongozi wa PIF wiki ijayo ili kupitia mwenendo wa timu na kupanga miradi ya miundombinu kama uwanja wa mazoezi na maendeleo ya uwanja wa nyumbani.

Klabu inaendelea kumuunga mkono kocha huyo, lakini inasisitiza umuhimu wa matokeo huku wakiwa na mechi tano za mwisho za kuwania nafasi za Ulaya.

Newcastle Wanapanga Mazungumzo na Howe huku Wakiangalia Uwezekano wa Kumuuza Gordon.

Kwa upande mwingine, wachambuzi kama Jamie Carragher na Dean Ashton wameonya kuwa Newcastle wanaweza kujikuta wakipambana na hatari ya kushuka daraja baada ya kupoteza 2-1 dhidi ya AFC Bournemouth, licha ya kuwa na pointi 42 kwa sasa.

Mpaka sasa Newcastle wapo nafasi ya 14 kwenye msimamo wa ligi, na mechi ijayo anatarajiwa kushuka dimbani kukipiga dhidi ya vinara wa ligi Arsenal.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.