Watu wote watakuwa wanakubali kuwa mshambuliaji wa Yanga, raia wa Zimbabwe Prince Dube, anapitia kipindi kigumu sana ndani ya Yanga, baada ya kukaa muda mrefu bila kupata bao.
Mbaya zaidi, wakati timu yake ikiwa inapambana kwenda makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, alikosa nafasi ya wazi iliyokuwa inamaliza kabisa mchezo kwa kuipa timu hiyo bao la tatu. Lakini ikashindikana na akaomba mwenyewe kutolewa.
Kufuatia hali hiyo, Afisa Habari wa Yanga, Ali Kamwe, ametoa ujumbe mzito wa kumtia nguvu mchezaji huyo kwenye kipindi hiki kigumu anachopitia.

Kamwe amesema: “Imani ni kwake Baba aliye juu Mbinguni, Prince.
“Kuna nyakati Mwanadamu unaweka sana jitihada kwenye Maisha, unavuja jasho lako lote, unatumia nguvu zako na uwezo wako wa kila aina, lakini mwisho wa siku haupati matokeo unayoyatamani.
“Inatokea hii Dube. Inaweza kumtokea Mkulima shambani, inaweza kumtokea Mama sokoni na inaweza kumtokea Ronaldo kwenye uwanja wa mpira.
“Inamtokea Yeyote. Kipindi unachopitia sasa hivi Dube uwanjani kinaweza kumtokea mwanadamu yeyote anayevuta pumzi ya Mungu duniani.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa.




